Maelezo ya Chini
a Ingawa malaika huyo hatajwi kwa jina, yaonekana ndiye yuleyule ambaye sauti yake ilisikiwa ikimwagiza Gabrieli amsaidie Danieli kuhusu lile ono ambalo alikuwa ametoka tu kuona. (Linganisha Danieli 8:2, 15, 16 na Danieli 12:7, 8.) Isitoshe, Danieli 10:13 huonyesha kwamba Mikaeli, “mmoja wa hao wakuu wa mbele,” alikuja kumsaidia malaika huyo. Kwa hiyo, malaika huyo asiyetajwa kwa jina lazima alikuwa na pendeleo la kufanya kazi bega kwa bega na Gabrieli na Mikaeli.