Maelezo ya Chini
a Ilionyeshwa kwamba mwanadamu aliumbwa mwaka wa 4128 na dhambi ikaingia mwaka wa 4126 B.C.E. Orodha hiyo ya tarehe ilifuata tafsiri ya hati yenye makosa ya Matendo 13:20 katika The Emphatic Diaglott, iliyosema kwamba Mungu aliwapa Israeli waamuzi “karibu miaka mia nne na hamsini, mpaka Samweli nabii.” Maelezo ya chini yalisema kwamba hii haikupatana na 1 Wafalme 6:1, ambapo herufi ya Kiebrania daleth (inayodhaniwa kuisimamia namba 4) ilidhaniwa kuwa hivyo badala ya herufi he (5). Kwa hiyo, ilishauriwa kwamba miaka 580 (si 480) ilikwisha kati ya kutoka kwa Israeli Misri na wakati ambao Sulemani alianza kulijenga hekalu la Yehova. Lakini hati za zamani kupita zote zinaonyesha namba zote. Kwa hiyo isingaliwezekana kuwe na kosa la mnakili katika 1 Wafalme 6:1, ambacho kinaonyesha kwa usahihi kipindi hiki kilikuwa miaka 480. Hii inapatana na kusoma kwa usahihi Matendo 13:20, panapoonyesha kwamba kipindi cha “karibu miaka mia nne na hamsini” kinachotajwa hapo kiliutangulia wakati wa Waamuzi.
Katika mwaka wa 1943 kitabu cha Watch Tower Society “The Truth Shall Make You Free” kiliiachilia mbali miaka ya ziada 100 isiyokuwapo kabisa katika kipindi cha Waamuzi na kuonyesha miaka 6,000 ya kuwako kwa mwanadamu itakwisha katika miaka ya kuanzia na wa 1970. Pia kilikuthibitisha kuanza kwa kuwapo kwa Kristo katika mwaka wa 1914 C.E., si mwaka wa 1874.