Maelezo ya Chini
b Ukurasa wa 230, mistari 12-14, unasema: “Kwa hiyo walikuwa wametiwa chachu, kwa sababu matoleo ya hadhara ya Israeli ya shukrani, hata patakatifu zaidi sana, yametiwa chachu na kutokamilika na dhambi nayo yanahitaji toleo la dhambi.”
Kulingana na yaliyotangulia, tunasoma katika kitabu Biblical Commentary on The Old Testament, kilichoandikwa na Keil na Delitzsch, (Volume II-The Pentateuch) na chini ya kichwa kidogo (ukurasa 437) kinachosema “Kutakaswa kwa Sabato na Sikukuu ya Yehova.—Sura ya XXIII,” na katika mistari ya 16-34 ukurasa 443, yafuatayo:
“‘. . . Mst. 20. Kuhani atawapunga (wana-kondoo wawili wa matoleo ya amani), pamoja na mikate ya malimbuko, kama toleo la kupungwa mbele za pamoja na wana-kondoo wawili (wawili wale ambao wametajwa sasa hivi), hiyo (mikate) itakuwa kwa Yehova ikitolewa na kuhani.’ . . . Toleo la dhambi lilipaswa kuamsha mawazo ya ndani ya kundi la Israeli wajue ni wenye dhambi, ili wanapokula mkate wao wa kila siku wenye chachu wasitumikie chachu ya hali yao zamani, bali wamwombe na kumsihi Bwana wao Mungu awasamehe na kuwaondolea dhambi yao.”