Maelezo ya Chini
a Maneno ya lugha ya awali ya Biblia yaliyotafsiriwa “roho” yana maana ya msingi ya “pumzi.” Maana pana inarejelea kitu ambacho hakiwezi kuonekana lakini ambacho kina nguvu inayodhihirika. Biblia inamfafanua Mungu kuwa Mtu Mkuu Zaidi wa Roho. Mtu wa kiroho huchagua kuongozwa na mapenzi ya Mungu na roho takatifu ya Mungu.