Maelezo ya Chini
b Inawezekana kwamba waandishi wa Biblia Wakristo walitumia jina la Mungu waliponukuu maandishi ya “Agano la Kale” yaliyokuwa na jina hilo. Kitabu The Anchor Bible Dictionary kinasema: “Kuna uthibitisho unaoonyesha kwamba Tetragramatoni, Jina la Mungu, Yahweh ilipatikana katika baadhi ya manukuu ya A[gano] la K[ale] katika A[gano] J[ipya] wakati maandiko ya [Agano Jipya] yalipokuwa yakiandikwa kwa mara ya kwanza.” (Buku la 6, ukurasa 392) Ili kupata habari zaidi, ona Nyongeza A5 yenye kichwa “Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo” katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Nyongeza ya C2 katika Toleo la funzo la Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya la Kiingereza, ina orodha ya tafsiri za Biblia zinazotumia jina hilo takatifu kwenye Waroma 10:13.