Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatano, Septemba 17

Wenye furaha ni wale ambao matendo yao ya kuasi sheria yamesamehewa na ambao dhambi zao zimefunikwa.—Rom. 4:7.

Mungu anasamehe au kufunika dhambi za wale wanaoweka imani kwake. Anawasamehe kabisa na hatahesabu dhambi zao kamwe. (Zab. 32:​1, 2) Yehova anawaona watu hao kuwa hawana hatia na waadilifu kwa msingi wa imani yao. Ingawa Abrahamu, Daudi, na waabudu wengine waaminifu wa Mungu walitangazwa kuwa waadilifu, bado walikuwa watenda dhambi wasio wakamilifu. Lakini kwa sababu ya imani yao, Mungu aliwaona kuwa wasio na hatia hasa alipowalinganisha na wale ambao hawakuwa na imani kwake. (Efe. 2:12) Kama mtume Paulo anavyoeleza waziwazi kwenye barua yake, ni lazima mtu awe na imani ili kuwa na uhusiano wa kibinafsi pamoja na Mungu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Abrahamu na Daudi, na ni hivyo kwetu pia. w23.12 3 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Septemba 18

Sikuzote na tumtolee Mungu dhabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo yetu ambalo hulitangaza jina lake hadharani.—Ebr. 13:15.

Leo, Wakristo wote wana pendeleo la kumtolea Yehova dhabihu kwa kutumia wakati, nguvu, na mali zao, ili kuendeleza kazi ya Ufalme wa Mungu. Tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini pendeleo letu la kumwabudu Yehova kwa kumtolea dhabihu zetu zilizo bora kabisa. Mtume Paulo anataja mambo mbalimbali kuhusu ibada yetu ambayo hatupaswi kamwe kuyapuuza. (Ebr. 10:​22-25) Mambo hayo yanatia ndani kumkaribia Yehova katika sala, kutoa tangazo la hadharani la tumaini letu, kukutana pamoja tukiwa kutaniko, na kutiana moyo “zaidi kwa kadiri [tunavyoona] siku ile [ya Yehova] ikikaribia.” Karibu na mwisho wa simulizi la Ufunuo, malaika wa Yehova anasema maneno yafuatayo mara mbili ili kusisitiza: “Mwabudu Mungu!” (Ufu. 19:10; 22:9) Acheni tuendelee kukumbuka kweli hizi zenye kina za kiroho kuhusu hekalu kubwa la kiroho la Yehova na pendeleo letu lenye thamani la kumwabudu Mungu wetu Mkuu! w23.10 29 ¶17-18

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Septemba 19

Tuendelee kupendana.—1 Yoh. 4:7.

Sote tunataka ‘kuendelea kupendana.’ Hata hivyo, ni muhimu kukumbuka kwamba Yesu alionya kuwa “upendo wa wengi [ungepoa].” (Mt. 24:12) Yesu hakumaanisha kwamba wanafunzi wake wengi wangeacha kupendana. Hata hivyo, tunapaswa kuwa makini ili tusiathiriwe na mtazamo wa ulimwengu wa kutopendana. Tukiwa na wazo hilo akilini, acheni tujiulize swali hili muhimu: Je, kuna njia yoyote ya kupima ikiwa upendo wetu kwa ndugu zetu una nguvu au ni dhaifu? Njia moja ya kupima ikiwa upendo wetu una nguvu au ni dhaifu ni kwa kuchunguza jinsi tunavyoshughulikia hali fulani maishani. (2 Kor. 8:8) Mojawapo ya hali hizo inatajwa na mtume Petro, alisema hivi: “Zaidi ya mambo yote, pendaneni sana, kwa sababu upendo hufunika dhambi nyingi.” (1 Pet. 4:8) Hivyo, udhaifu na kutokamilika kwa wengine kunaweza kujaribu upendo wetu. w23.11 10-11 ¶12-13

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki