Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Siku za Kumalizia za J. F. Rutherford

      Ndugu Rutherford alikuwa amepatwa na kansa kwenye sehemu ya mwisho ya utumbo mpana na afya yake ilikuwa mbaya wakati wa mkusanyiko wa St. Louis. Hata hivyo, yeye aliweza kutoa hotuba tano zenye nguvu. Lakini baada ya mkusanyiko huo, hali yake ilizidi kuwa mbaya, naye akalazimika kupasuliwa sehemu ya mwisho ya utumbo mpana. Arthur Worsley akumbuka siku ambayo Ndugu Rutherford alisema kwaheri kwa familia ya Betheli. “Alitufunulia siri kwamba atafanyiwa upasuaji hatari na kwamba kama atapona au sivyo, alikuwa na hakika kwamba sisi tungeendelea kupiga mbiu ya jina la Yehova. Yeye . . . alimalizia kwa kusema, ‘Hivyo, Mungu akipenda, nitawaona tena. Ikiwa sivyo, endeleeni kupiga vita.’ Kila jicho katika familia lilikuwa na machozi.”

      Ndugu Rutherford, mwenye umri wa miaka 72, aliokoka upasuaji ule. Upesi baada ya hapo alipelekwa kwenye makao katika California ambayo alikuwa ameyaita Beth-Sarim. Ilikuwa wazi kwa wapendwa wake, na kwa wastadi wa kitiba, kwamba hangepona. Kwa kweli, alihitaji upasuaji zaidi.

      Karibu katikati ya Desemba, Nathan H. Knorr, Frederick W. Franz, na Hayden C. Covington waliwasili kutoka Brooklyn. Hazel Burford, aliyemtunza Ndugu Rutherford wakati wa siku hizo zenye huzuni na zenye kujaribu, alikumbuka baadaye: “Walitumia siku kadhaa pamoja naye wakipitia ripoti ya mwaka kwa ajili ya Kitabu-Mwaka na mambo mengine ya kitengenezo. Baada ya wao kuondoka, Ndugu Rutherford aliendelea kuwa dhaifu na, kama majuma matatu baadaye, Alhamisi, Januari 8, 1942, alimaliza mwendo wake wa kidunia kwa uaminifu.”i

      Habari ya kifo cha Ndugu Rutherford ilipokewaje katika Betheli? “Mimi sitasahau siku ile tulipopata kujua juu ya kifo cha Ndugu Rutherford,” akakumbuka William A. Elrod, aliyekuwa amekuwa mshiriki wa familia ya Betheli kwa miaka tisa. “Ilikuwa wakati wa adhuhuri familia ilipokusanyika kwa ajili ya chakula cha mchana. Tangazo lilikuwa fupi. Hakukuwa na hotuba zozote. Hakuna mtu aliyepumzika siku hiyo ili kuomboleza. Badala yake, tulirudi kwenye kiwanda na kufanya kazi kwa bidii zaidi kuliko tulivyopata kufanya.”

      Hizo zilikuwa nyakati ngumu kwelikweli kwa Mashahidi wa Yehova. Vita ilikuwa imekuwa pigano la duniani pote. Mapigano yalienea kutoka Ulaya hadi Afrika, halafu kwenye ile iliyokuwa inajulikana wakati huo kuwa Muungano wa Sovieti. Katika Desemba 7, 1941, mwezi mmoja tu kabla ya kifo cha Ndugu Rutherford, shambulio la Japani juu ya Pearl Harbor lilikuwa limeingiza Marekani vitani. Katika mahali pengi Mashahidi walikuwa shabaha ya jeuri ya wafanyaghasia na namna nyinginezo za mnyanyaso mkali.

      Ingekuwaje sasa?

  • Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Sura ya 8

      Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)

      “KWA WAPENDA THEOKRASI WOTE:

      Katika Januari 8, 1942, ndugu yetu mpendwa, J. F. Rutherford, alimaliza mwendo wake wa kidunia kwa uaminifu . . . Ilikuwa shangwe na faraja kwake kuona na kujua kwamba mashahidi wote wa Bwana wanafuata, si binadamu yeyote, bali Mfalme Kristo Yesu akiwa Kiongozi wao, na kwamba watasonga mbele na kazi kwa umoja kamili wa tendo.”—Barua yenye kutangaza kifo cha Ndugu Rutherford.a

      HABARI za kifo cha Ndugu Rutherford zilifika zikiwa mshtuko wa kitambo kwa Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Wengi walijua kwamba alikuwa amekuwa mgonjwa, lakini hawakutarajia afe upesi hivyo. Walihuzunishwa na kifo cha ndugu yao mpendwa lakini walikuwa wameazimia “kusonga mbele na kazi”—kazi ya kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu. Wao hawakumwona J. F. Rutherford kuwa kiongozi wao. Charles E. Wagner, ambaye alikuwa amefanya kazi katika ofisi ya Ndugu Rutherford, alionelea hivi: “Akina ndugu kila mahali walikuwa wamesitawisha usadikisho imara kwamba kazi ya Yehova haikutegemea binadamu yeyote.” Hata hivyo, mtu fulani alihitajiwa ili abebe madaraka ambayo Ndugu Rutherford alikuwa amebeba akiwa msimamizi wa Watch Tower Society.

      “Tumeazimia Kukaa Karibu na Bwana”

      Ilikuwa tamaa ya moyoni ya Ndugu Rutherford kwamba Mashahidi wa Yehova wajulishe habari njema bila kuacha. Kwa hiyo katikati ya Desemba 1941, majuma kadhaa kabla ya kifo chake, aliita pamoja waelekezi wanne wa yale mashirika mawili makuu yaliyo halali yaliyotumiwa na Mashahidi wa Yehova na kudokeza kwamba upesi kadiri iwezekanavyo baada ya kifo chake, washiriki wote wa mabaraza ya waelekezi waitwe katika kikao cha pamoja na kuchagua msimamizi na makamu wa msimamizi.

      Alasiri ya Januari 13, 1942, siku tano tu baada ya kifo cha Rutherford, washiriki wote wa baraza la mashirika hayo mawili walikutana pamoja kwenye Betheli ya Brooklyn. Siku kadhaa mapema, makamu wa msimamizi wa Sosaiti, Nathan H. Knorr mwenye umri wa miaka 36, alikuwa amedokeza kwamba watafute kwa moyo wa bidii hekima ya kimungu kwa sala na kutafakari. Washiriki wa baraza walitambua kwamba ingawa ndugu aliyechaguliwa awe msimamizi angesimamia mambo ya kisheria ya Watch Tower Society, pia angetumikia akiwa mwangalizi mkuu wa tengenezo. Ni nani aliyekuwa na sifa za kiroho zilizohitajiwa kwa daraka hilo zito katika kuangalia kazi ya Yehova? Mkutano huo wa pamoja ulifunguliwa kwa sala, na baada ya ufikirio wa uangalifu, Ndugu Knorr alichaguliwa kwa umoja awe msimamizi wa mashirika yote mawili na Hayden C. Covington mwenye umri wa miaka 30, aliyekuwa wakili wa Sosaiti, akachaguliwa kuwa makamu wa msimamizi.b

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki