-
Kimbelembele Hutokeza AibuMnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 1
-
-
16. Ni katika njia gani Sauli alikosa subira?
16 Lakini, baadaye Sauli akakosa kuwa mwenye kiasi. Alipokuwa akipigana na Wafilisti, alirudi Gilgali, ambako alitazamiwa amngojee Samweli aje amsihi Mungu kwa dhabihu. Samweli alipochelewa kufika kwa wakati uliopangwa, kwa kimbelembele Sauli mwenyewe akatoa dhabihu ya kuteketezwa. Alipomaliza tu, Samweli akafika. “Umefanya nini?” Samweli akamwuliza. Sauli akajibu: “Ni kwa sababu naliona ya kuwa watu wanatawanyika mbali nami, na wewe hukuja siku zile zilizonenwa . . . Kwa hiyo nalijishurutisha, nikatoa sadaka ya kuteketezwa.”—1 Samweli 13:8-12.
17. (a) Ukitazama kijuujuu tu, kwa nini matendo ya Sauli huenda yakaonekana kuwa yalifaa? (b) Kwa nini Yehova alimkemea Sauli kwa kukosa subira?
17 Ukitazama kijuujuu tu, huenda matendo ya Sauli yakaonekana kuwa yalifaa. Kwani, watu wa Mungu walikuwa “katika dhiki,” na ‘kufadhaishwa,’ wakitetemeka kwa sababu ya hali mbaya waliyokabili. (1 Samweli 13:6, 7) Si vibaya kuchukua hatua ikihitajika.d Lakini, kumbuka kwamba Yehova anaweza kusoma mioyo na kutambua nia zetu za ndani kabisa. (1 Samweli 16:7) Kwa hiyo, huenda aliona mambo fulani kuhusu Sauli ambayo hayatajwi moja kwa moja katika masimulizi hayo ya Biblia. Kwa mfano, huenda Yehova aliona kwamba Sauli alikosa subira kwa sababu ya kiburi. Labda Sauli alikasirika sana kwamba yeye—mfalme wa Israeli yote—ati amngoje mtu ambaye alimwona kuwa nabii aliyezeeka, mwenye kuchelewa-chelewa! Kwa vyovyote vile, Sauli alihisi kwamba kuchelewa kwa Samweli kulimpa haki ya kujifanyia mambo mwenyewe na kupuuza maagizo ya wazi ambayo alikuwa amepewa. Matokeo yakawaje? Samweli hakumsifu Sauli kwa hatua aliyochukua. Badala yake, alimkemea akisema: “Ufalme wako hautadumu . . . kwa sababu wewe hukulishika neno lile BWANA alilokuamuru.” (1 Samweli 13:13, 14) Kwa mara nyingine tena, kimbelembele kilitokeza aibu.
-
-
Kimbelembele Hutokeza AibuMnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 1
-
-
d Kwa mfano, Finehasi alichukua hatua ya haraka ili kukomesha pigo ambalo lilikuwa limeua makumi ya maelfu ya Waisraeli, naye Daudi aliwatia moyo watu wake wenye njaa sana wale pamoja naye mikate ya wonyesho katika “nyumba ya Mungu.” Mungu hakuyashutumu matendo hayo mawili kuwa kimbelembele.—Mathayo 12:2-4; Hesabu 25:7-9; 1 Samweli 21:1-6.
-