-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2006 | Januari 1
-
-
Maswali Kutoka kwa Wasomaji
Zaburi 102:26 inasema kwamba dunia na mbingu “zitaangamia.” Je, hilo linamaanisha kwamba Dunia itaharibiwa?
Mtunga-zaburi alisema hivi aliposali kwa Yehova: “Wewe uliiweka misingi ya dunia zamani za kale, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako. Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama; nazo zote zitachakaa kama vazi. Utazibadili kama mavazi, nazo zitamaliza zamu yake.” (Zaburi 102:25, 26) Muktadha unaonyesha kwamba mistari hiyo inazungumzia hali ya Mungu ya kuwapo milele, bali si uharibifu wa dunia. Pia, muktadha unaonyesha jinsi ukweli huo muhimu unavyowafariji watumishi wa Mungu.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2006 | Januari 1
-
-
Lakini, hata miaka mingi ambayo dunia na mbingu zimekuwapo haiwezi kulinganishwa na hali ya Yehova ya kuwapo milele. Mtunga-zaburi anaendelea kusema hivi: “Hizo [dunia na mbingu] zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama.” (Zaburi 102:26) Dunia na mbingu zinazoonekana zinaweza kuangamia. Naam, katika maandiko mengine Yehova alisema kwamba zitadumu milele. (Zaburi 119:90; Mhubiri 1:4) Lakini zingeweza kuharibiwa ikiwa hilo lingekuwa kusudi la Mungu. Hata hivyo, Mungu hawezi kufa. Uumbaji unaoonekana unaendelea ‘kusimama milele’ kwa sababu Mungu anautunza. (Zaburi 148:6) Ikiwa Yehova angeacha kurudisha upya uumbaji unaoonekana, basi uumbaji ‘wote ungechakaa kama vazi.’ (Zaburi 102:26) Kama vile mwanadamu anavyoishi kwa muda mrefu kuliko muda ambao mavazi yake yanadumu, ndivyo Yehova angeishi kwa muda mrefu kuliko muda ambao uumbaji wake utadumu—ikiwa angechagua kufanya hivyo. Hata hivyo, maandiko mengine yanatuonyesha kwamba hayo si mapenzi yake. Neno la Mungu linatuhakikishia kwamba Yehova ameamua dunia na mbingu halisi zidumu milele.—Zaburi 104:5.
-