Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
    Mkaribie Yehova
    • 3. Yehova anatualika tufanye nini, naye anatuahidi nini?

      3 Yehova anatualika tumkaribie. Yuko tayari na ana nia ya kutukubali kuwa rafiki zake. Vilevile, anaahidi kwamba tukijitahidi kumkaribia, atatukaribia pia. Kwa hiyo, tunaweza kufurahia jambo muhimu sana—kuwa ‘msiri wa BWANA.’a (Zaburi 25:14) Neno ‘-a siri’ latoa maana ya mazungumzo ya siri na rafiki wa karibu.

      4. Rafiki msiri ni rafiki wa aina gani, na Yehova huthibitikaje kuwa rafiki msiri kwa wale wanaomkaribia?

      4 Je, una rafiki msiri unayezungumza naye mambo yako ya siri? Huyo ni rafiki anayekujali. Unamtumaini kwa sababu amekuwa mwaminifu. Unafurahi hata zaidi unapomwambia mambo yanayokufurahisha. Anasikiliza kwa huruma unapomweleza mambo yanayokuhuzunisha na hivyo unapata utulivu. Hata inapoonekana kwamba hakuna mtu mwingine anayeelewa hali yako, yeye hukuelewa. Vivyo hivyo, unapomkaribia Mungu, unapata Rafiki wa pekee ambaye anakuthamini sana, anakujali sana, na kukuelewa kabisa. (Zaburi 103:14; 1 Petro 5:7) Unamtumaini na kumweleza hisia zako za moyoni, kwa kuwa unajua kwamba yeye ni mwaminifu kwa wale walio waaminifu kwake. (Zaburi 18:25, Biblia Habari Njema) Hata hivyo, Mungu ndiye ametuandalia fursa ya kuwa na urafiki wa karibu sana pamoja naye.

  • Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
    Mkaribie Yehova
    • a Jambo la kuvutia ni kwamba, neno la Kiebrania linalotafsiriwa ‘-a siri’ limetumiwa kwenye andiko la Amosi 3:7, lisemalo kwamba Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova huwafunulia watumishi wake “siri yake,” na kuwajulisha kimbele mambo anayokusudia kufanya.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki