-
Je, Utakuwepo Katika Ulimwengu Mpya?Mnara wa Mlinzi—2000 | Aprili 15
-
-
14, 15. Ni utendaji gani wenye kuthawabisha uwezao kutarajia kulingana na Isaya 65:21, 22?
14 Badala ya kuzungumzia sana jinsi mtenda-dhambi wa kukusudia awezavyo kuondolewa, Isaya afafanua hali za maisha zitakazokuwapo katika ulimwengu mpya. Jiwazie ukiwa katika hali hizo. Huenda mambo uwezayo kuwazia kwanza yakawa yale unayopenda sana. Isaya azungumzia mambo hayo katika mstari wa 21 na 22: “Watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.”
15 Ikiwa bado hujapata ujuzi wa kujenga au kulima, unabii wa Isaya wadokeza kwamba utaelimishwa. Hata hivyo, je, ungetaka kujifunza ukisaidiwa na wafunzi wenye uwezo, labda majirani wenye fadhili wanaofurahia kukusaidia? Isaya hakusema ikiwa nyumba yako itakuwa na madirisha makubwa yenye pazia na yasiyo na vioo ili kukuwezesha kufurahia kupunga upepo, au madirisha yenye vioo ambavyo kupitia hivyo waweza kuona majira yenye kubadilika-badilika. Je, utajenga nyumba yako ikiwa na paa yenye kuinama ili mvua na theluji zitiririke? Au tabia ya nchi ya kwenu itahitaji paa tambarare—kama mojawapo ya zile za Mashariki ya Kati—paa ambayo wewe na familia yako mwaweza kukusanyikia ili kula milo mizuri na kuwa na mazungumzo yenye kupendeza?—Kumbukumbu la Torati 22:8; Nehemia 8:16.
-
-
Je, Utakuwepo Katika Ulimwengu Mpya?Mnara wa Mlinzi—2000 | Aprili 15
-
-
Isaya 65:21 pia lasema kwamba utapanda na kula matunda. Ni wazi kwamba hilo laonyesha jinsi hali itakavyokuwa kwa ujumla. Utaridhishwa sana na jitihada zako, matokeo ya jasho lako mwenyewe.
-