-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia;
-
-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
37. Mamilioni leo waishije kana kwamba kuna njia kuu kati ya “Ashuru” na “Misri”?
37 Leo, mabaki ya Waisraeli watiwa-mafuta ni “baraka kati ya dunia.” Wao huendeleza ibada ya kweli nao wanawatangazia watu katika mataifa yote ujumbe wa Ufalme.
-
-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
38. (a) Israeli ‘atakuwaje wa tatu pamoja na Misri na Ashuru’? (b) Kwa nini Yehova asema “Wabarikiwe watu wangu”?
38 Hata hivyo, Israeli ‘apataje kuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru’? Mapema katika “wakati wa mwisho,” walio wengi wa wale wanaomtumikia Yehova duniani walikuwa washiriki wa “Israeli wa Mungu.” (Danieli 12:9; Wagalatia 6:16) Tangu miaka ya 1930, umati mkubwa wa “kondoo wengine,” walio na tumaini la kuishi duniani, umetokea. (Yohana 10:16a; Ufunuo 7:9) Huku wakitoka katika mataifa—yaliyowakilishwa na Misri na Ashuru—wamiminika kwenye nyumba ya ibada ya Yehova na kuwaalika wengine wajiunge nao. (Isaya 2:2-4) Wanafanya kazi ileile ya kuhubiri kama ndugu zao watiwa-mafuta, huvumilia majaribu yaleyale, hudhihirisha uaminifu na uaminifu-maadili uleule, nao hujilisha kwenye meza ileile ya kiroho. Kwa kweli, watiwa-mafuta na “kondoo wengine” ni “kundi moja, mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16b)
-