Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Babeli Umeanguka”!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Na, tazama, linakuja kundi [“gari la vita,” “NW”] la watu, wapanda farasi, wakienda wawili wawili.” (Isaya 21:8, 9a)

  • “Babeli Umeanguka”!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 13, 14. (a) Babiloni la kale lapatwa na nini, na sanamu zake zavunjwaje? (b) Babiloni Mkubwa alipatwaje na anguko kama hilo, nalo lilitukia lini?

      13 Mlinzi kwenye maono ya Isaya aona gari la vita likija. Kuna habari gani? “Akajibu na kusema, Babeli umeanguka, umeanguka; na sanamu zote za miungu yake zimevunjwa chini”! (Isaya 21:9b) Ripoti hiyo yasisimua kama nini! Mwishowe, mwenye hila huyo anayeharibu watu wa Mungu ameanguka!c Hata hivyo, mifano na sanamu za Babiloni zavunjwaje? Je, wavamizi wa Umedi na Uajemi wataingia katika mahekalu ya Babiloni na kuvunja-vunja sanamu zake nyingi? La, jambo hilo halihitajiki. Miungu ya sanamu ya Babiloni itavunjwa kwa njia ya kwamba itaonyeshwa kuwa isiyo na uwezo wa kulinda jiji hilo. Na Babiloni ataanguka wakati anaposhindwa kuendelea kuwaonea watu wa Mungu.

      14 Namna gani Babiloni Mkubwa? Alipopanga njama ya kuonea watu wa Mungu wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, kwa kweli aliwashikilia uhamishoni kwa muda fulani. Kazi yao ya kuhubiri ilikaribia kukomeshwa kabisa. Msimamizi na maofisa wengine mashuhuri wa Watch Tower Society walifungwa gerezani kwa mashtaka ya uwongo. Lakini kukawa na mabadiliko yenye kushangaza mwaka wa 1919. Maofisa hao walifunguliwa kutoka gerezani, ofisi ya makao makuu ikafunguliwa tena, na kazi ya kuhubiri ikaanzishwa tena. Kwa hiyo, Babiloni Mkubwa alianguka kwa njia ya kwamba mshiko wake juu ya watu wa Mungu ulivunjwa.d Katika Ufunuo, malaika atangaza anguko hilo mara mbili akitumia maneno ya tangazo lililo kwenye Isaya 21:9.—Ufunuo 14:8; 18:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki