Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wokovu kwa Wanaochagua Nuru
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 1
    • Kulindwa Nyakati za Hatari

      16, 17. (a) Katika mwaka wa 539 K.W.K., Wayahudi walihitaji kufanya nini ili kuokoka anguko la Babiloni? (b) Huenda “vyumba vya ndani” vyafananisha nini leo, navyo hutunufaishaje?

      16 Watumishi wa Yehova wanahitaji ulinzi wake sikuzote. Hata hivyo, hivi karibuni atanyoosha mkono wake mara ya mwisho dhidi ya ulimwengu wa Shetani, nao waabudu wake watahitaji msaada wake kuliko wakati mwingine wowote. (1 Yohana 5:19) Kuhusu wakati huo wa hatari, Yehova atuonya hivi: “Njoni, watu wangu, ingia wewe ndani ya vyumba vyako [“vyumba vya ndani,” NW], ukafunge mlango nyuma yako ujifiche kitambo kidogo, mpaka ghadhabu hii itakapopita.

  • Wokovu kwa Wanaochagua Nuru
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 1
    • Isaya 26:20,

  • Wokovu kwa Wanaochagua Nuru
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 1
    • Onyo hili lilionyesha Wayahudi jinsi ya kuokoka anguko la Babiloni mwaka wa 539 K.W.K. Wale waliotii onyo hilo wangekaa katika nyumba zao, wakiwa salama bila kusumbuliwa na majeshi yenye kushinda yaliyokuwa barabarani.

      17 Leo, “vyumba vya ndani” vinavyotajwa katika unabii huo huenda vyafananisha makumi ya maelfu ya makutaniko ya watu wa Yehova ulimwenguni pote. Makutaniko hayo ni ulinzi hata sasa, ni mahali ambapo Wakristo hupata usalama miongoni mwa ndugu zao, chini ya uangalizi wenye upendo wa wazee. (Isaya 32:1, 2; Waebrania 10:24, 25) Ni kweli hasa tunapozingatia jinsi ambavyo mwisho wa mfumo huu wa mambo umekaribia wakati ambapo wokovu utategemea utii.—Sefania 2:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki