-
Paradiso Yarudishwa!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Watu wa Yehova Wafurahi
17. Unabii wa Isaya wamalizikia kwa masimulizi gani yenye furaha?
17 Sura ya 35 ya unabii wa Isaya yamalizikia kwa masimulizi yenye furaha: “Hao waliokombolewa na BWANA watarudi, watafika Sayuni wakiimba; na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia.” (Isaya 35:10) Huenda mateka Wayahudi walioutegemea unabii huo ili kupata faraja na tumaini wakiwa uhamishoni walihangaikia jinsi ambavyo mambo mbalimbali ya unabii yangetimizwa. Labda hawajaelewa mambo mengi yanayotiwa ndani katika unabii huo. Licha ya hayo, imekuwa wazi sana kwamba “watarudi, watafika Sayuni.”
18. Huzuni na majonzi huko Babiloni zabadilikaje kuwa shangwe na furaha katika nchi iliyorudishwa?
18 Basi, katika mwaka wa 537 K.W.K., wanaume wapatao 50,000 (ikijumlisha watumwa zaidi ya 7,000) pamoja na wanawake na watoto wafunga safari ya miezi minne kurudi Yerusalemu, wakimtumaini Yehova kabisa. (Ezra 2:64, 65) Miezi michache tu baadaye, madhabahu ya Yehova yajengwa, ambayo ni hatua ya kwanza kuelekea ujenzi kamili wa hekalu. Unabii wa Isaya ambao umedumu miaka 200 watimia. Badala ya huzuni na majonzi ya taifa hilo huko Babiloni, sasa ni shangwe na furaha katika nchi iliyorudishwa. Yehova ametimiza ahadi yake. Paradiso—paradiso halisi na ya kiroho vilevile—imerudishwa!
Kuzaliwa kwa Taifa Jipya
19. Kwa nini twaweza kusema kwamba unabii wa Isaya una utimizo wa kiasi tu katika karne ya sita K.W.K.?
19 Hapana budi utimizo wa unabii wa Isaya sura ya 35 ni wa kiasi tu katika karne ya sita K.W.K. Hali za kiparadiso wanazofurahia Wayahudi waliorudishwa ni za muda tu. Baadaye, mafundisho ya kidini yasiyo ya kweli na uzalendo zachafua ibada safi. Wayahudi wapata tena huzuni na majonzi ya kiroho. Hatimaye Yehova awakataa wasiwe watu wake. (Mathayo 21:43) Furaha yao haidumu kwa sababu ya kutotii ambako kumetokea tena. Hayo yote yaonyesha kuwepo kwa utimizo mwingine ulio mkubwa zaidi wa Isaya sura ya 35.
-
-
Paradiso Yarudishwa!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Sauti ya furaha ilisikika huku habari njema za Ufalme wa Mungu zikihubiriwa. Majuma saba baada ya kufa na kufufuliwa, Yesu aliyetukuzwa alianzisha kutaniko la Kikristo, Israeli la kiroho linalojumlisha Wayahudi na watu wengine waliokombolewa na damu ya Yesu iliyomwagwa, wakazaliwa kuwa wana wa kiroho wa Mungu na ndugu za Yesu, na kutiwa-mafuta kwa roho takatifu.—Matendo 2:1-4; Waroma 8:16, 17; 1 Petro 1:18, 19.
-
-
Paradiso Yarudishwa!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Jambo la maana zaidi ni kwamba wenye mioyo minyofu waliponyoka kutoka dini isiyo ya kweli nao wakaanza kufurahia paradiso ya kiroho katika kutaniko la Kikristo. (Isaya 52:11; 2 Wakorintho 6:17) Kama ilivyokuwa kwa Wayahudi waliokuwa wakirudi kutoka Babiloni, hao walioponyoka walitambua uhitaji wa roho nzuri na yenye ujasiri.—Waroma 12:11.
-