-
Faraja kwa Watu wa MunguUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
2. (a) Yehova anamtumia Isaya kuelekeza ujumbe wake wa faraja kwa nani? (b) Wayahudi waaminifu ‘wanafuatiaje uadilifu’?
2 Yehova anawaambia hivi wale walio katika Yuda wanaoelekeza mioyo yao kwake: “Nisikilizeni, ninyi mnaoifuatia haki [“uadilifu,” “NW”]; ninyi mnaomtafuta BWANA.” (Isaya 51:1a) ‘Kufuatia uadilifu’ kunamaanisha kuchukua hatua. Wale ‘wanaofuatia uadilifu’ hawatadai kwa maneno tu kwamba wao ni watu wa Mungu. Watajitahidi sana kuwa waadilifu na kuishi kupatana na mapenzi ya Mungu. (Zaburi 34:15; Mithali 21:21) Watamtegemea Yehova kuwa Chanzo pekee cha uadilifu, na ‘watamtafuta BWANA.’ (Zaburi 11:7; 145:17) Hiyo haimaanishi kuwa wanafanya hivyo kwa sababu hawajamjua Yehova au hawajui jinsi ya kumkaribia katika sala. Inamaanisha kuwa watajitahidi kumkaribia zaidi, kumwabudu, kumpelekea sala, na kutafuta mwelekezo wake katika yote wayafanyayo.
3, 4. (a) Ni nani “mwamba” ambao Wayahudi walichongwa kutokana nao, na ni nani “tundu la shimo” ambamo walichimbuliwa? (b) Kwa nini Wayahudi watafarijika kwa kuikumbuka asili ya uzawa wao?
3 Hata hivyo, wenye kufuatia uadilifu kweli kweli ni wachache katika Yuda kwa kulinganishwa na idadi iliyoko, na hiyo huenda ikawatia woga na hali ya kukata tamaa. Kwa hiyo Yehova anatumia kielezi cha machimbo ya mawe kuwatia moyo: “Uangalieni mwamba ule ambao mlitolewa kwa kuchongwa, na tundu la shimo ambalo mlitolewa kwa kuchimbuliwa.
-
-
Faraja kwa Watu wa MunguUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Mwamba” ambao Wayahudi walichongwa kutokana nao ni Abrahamu, mtu maarufu kihistoria ambaye taifa la Israeli hujivunia. (Mathayo 3:9; Yohana 8:33, 39) Yeye ndiye mzazi, yaani mwanadamu aliye chanzo cha taifa hilo. Sara ndiye “tundu la shimo,” alimotoka Isaka babu wa kale wa Israeli.
-
-
Faraja kwa Watu wa MunguUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
5. (a) Abrahamu na Sara wanafananisha nani? Eleza. (b) Katika utimizo wa mwisho, ni nani wanaofuatilia asili yao hadi kuufikia “mwamba”?
5 Inaelekea kuwa uchimbaji wa mfano unaotajwa katika Isaya 51:1, 2 una matumizi zaidi. Kumbukumbu la Torati 32:18, NW, humwita Yehova “Mwamba” aliyezaa Israeli na “yule Mwenye kumtokeza [Israeli] kwa utungu wa kuzaa.” Katika usemi huo wa mwisho, kitenzi cha Kiebrania kilichotumiwa hapo ni kama kile kinachoonekana kwenye Isaya 51:2 kuhusu Sara akizaa Israeli. Hivyo basi, Abrahamu ni mfano wa unabii wa kumfananisha Yehova, yule Abrahamu Mkubwa Zaidi. Sara, mke wa Abrahamu, anafananisha vema tengenezo la Yehova la kimbingu la ulimwengu mzima wa viumbe-roho, wanaoonyeshwa katika Maandiko Matakatifu kuwa mke, au mwanamke, wa Mungu. (Mwanzo 3:15; Ufunuo 12:1, 5) Katika utimizo wa mwisho wa maneno haya ya unabii wa Isaya, taifa linalozuka kutokana na ule “mwamba” ni “Israeli wa Mungu,” lile kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta, lililozaliwa Pentekoste 33 W.K. Kama vile ilivyozungumziwa katika sura zilizotangulia za kitabu hiki, taifa hilo liliingia katika utekwa wa Kibabiloni mwaka wa 1918 lakini likarudishwa kwenye hali ya ufanisi wa kiroho mwaka wa 1919.—Wagalatia 3:26-29; 4:28; 6:16.
-