-
Yule Mwanamke Tasa AshangiliaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watawamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu.
-
-
Yule Mwanamke Tasa AshangiliaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
11. (a) “Mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alibarikiwaje mwaka wa 1914? (Ona kielezi-chini.) (b) Kuanzia mwaka wa 1919 na kuendelea, watiwa-mafuta walio duniani wamepata baraka gani?
11 Yerusalemu la kidunia lilibarikiwa kwa kupata wakati wa kujengwa upya jinsi hiyo baada ya ule uhamisho wa Kibabiloni. “Yerusalemu la juu” limebarikiwa hata zaidi.a Hasa tangu mwaka wa 1919, “wazao” wake watiwa-mafuta wamechanuka katika hali yao ya kiroho iliyorudishwa. (Isaya 61:4; 66:8) ‘Waliwamiliki mataifa’ katika maana ya kwamba walienea wakaingia nchi nyingi kuwatafuta wale ambao wangetaka kujiunga na familia yao ya kiroho. Matokeo ni kwamba, ukuzi mkubwa ulivuvumka kwa kukusanya wale wana watiwa-mafuta. Idadi yao ya mwisho ya 144,000 ilionekana kuwa imejazwa wakati fulani katikati ya ile miaka ya 1930. (Ufunuo 14:3) Wakati huo, kukusanywa kwa watiwa-mafuta kuliacha kuwa lengo kuu la kazi ya kuhubiri. Hata hivyo, mpanuko haukukoma eti kwa sababu mkusanyo wa watiwa-mafuta ulikoma.
12. Ni nani zaidi ya watiwa-mafuta ambao wamekusanywa wakaingizwa katika kutaniko la Kikristo tangu miaka ya 1930?
12 Yesu mwenyewe alitabiri kwamba licha ya yeye kuwa na “kundi dogo” la ndugu watiwa-mafuta, angekuwa pia na “kondoo wengine” ambao ni lazima waletwe ndani ya zizi la kondoo la Wakristo wa kweli. (Luka 12:32; Yohana 10:16) Ingawa waandamani hao waaminifu wa watiwa-mafuta hawamo miongoni mwa wana watiwa-mafuta wa “Yerusalemu la juu,” wanatimiza sehemu muhimu iliyotajwa na unabii zamani. (Zekaria 8:23) Kuanzia miaka ya 1930 hadi leo, “umati mkubwa” wa waandamani hao umekusanywa, matokeo yakawa ni mpanuko usio na kifani wa kutaniko la Kikristo. (Ufunuo 7:9, 10) Leo huo umati mkubwa una mamilioni ya watu. Mpanuko wote huo umetokeza uharaka wa kuongeza Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, na ofisi za tawi. Maneno ya Isaya yanaonekana yamezidi kufaa sana. Ni pendeleo kama nini kuwa sehemu ya mpanuko huo uliotabiriwa!
-