-
Yehova Anachukia Ukosefu wa HakiMnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 1
-
-
Tunapata jibu katika andiko la Ezekieli 22:6, 7, 31.—Soma.
-
-
Yehova Anachukia Ukosefu wa HakiMnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 1
-
-
Katika Sheria aliyowapa Waisraeli, Yehova alitaja waziwazi kwamba watu wenye mamlaka hawakupaswa kutumia mamlaka yao vibaya. Angelibariki taifa hilo ikiwa tu viongozi wao wangewajali na kuwatendea watu wa hali ya chini kwa fadhili. (Kumbukumbu la Torati 27:19; 28:15, 45) Hata hivyo, katika siku za Ezekieli, wakuu huko Yerusalemu na Yuda walitumia vibaya mamlaka yao kwa njia za uovu. Walikuwa wakifanya nini?
Wakuu hao walitumia ‘mkono wao kumwaga damu.’ (Mstari wa 6) Neno “mkono” linawakilisha nguvu au mamlaka. Hivyo, tafsiri nyingine inasema: “Wakuu wa Israeli . . . wametumia nguvu zao kumwaga damu.” Kunawezaje kuwa na haki ikiwa viongozi ambao wanapaswa kudumisha na kuendeleza ufuataji wa sheria wanatumia vibaya nguvu na kuwaua watu wasio na hatia?
-