-
Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” YetuMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
Ezekieli anapopata kujua juu ya miti ambayo ingekua kando-kando ya mto huo, aambiwa: “Majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayatatindika kamwe; . . . na matunda yake yatakuwa chakula; na majani yake yatakuwa ni dawa.” Kwa nini miti hiyo huzaa kwa njia hii yenye kustaajabisha? “Kwa sababu maji yake yanatoka mahali patakatifu.” (Ezekieli 47:12b) Miti hiyo ya mfano hufananisha kimbele maandalizi yote ya Mungu kwa ajili ya kurudisha wanadamu kwenye ukamilifu kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Yesu. Hapa duniani wakati huu, baki la watiwa-mafuta huongoza katika kuandaa lishe na ponyo la kiroho. Baada ya wale 144,000 wote kupokea thawabu yao ya kimbingu, faida zinazotokana na utumishi wao wa kikuhani wakiwa watawala-wenzi pamoja na Kristo zitaenea hadi wakati ujao, hatimaye zikiongoza kwenye kushindwa kabisa kwa kifo cha Kiadamu.—Ufunuo 5:9, 10; 21:2-4.
-
-
Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” YetuMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
17, 18. (a) Mto unaotokeza uhai unafafanuliwaje kwenye Ufunuo 22:1, 2, na wakati muhimu wa utimizo wa ono hilo ni lini? (b) Ni kwa nini mto huo wa maji ya uhai utaingia kipindi cha mpanuko ulio mkubwa zaidi katika Paradiso?
17 Kwa kweli, ndipo mto ambao Ezekieli aliona utatiririka kwa maji ya uhai yenye nguvu nyingi. Huo ndio wakati muhimu wa utimizo wa unabii uliorekodiwa kwenye Ufunuo 22:1, 2: “Akanionyesha mto wa maji ya uhai, mwangavu kama fuwele, ukitiririka kutoka katika kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kuteremka katikati ya njia pana yalo. Na upande huu wa mto na upande ule kulikuwa na miti ya uhai yenye kutokeza mazao kumi na mawili ya matunda, ikitoa matunda yayo kila mwezi. Na majani ya hiyo miti yalikuwa ya kuponya mataifa.”
18 Wakati wa Milenia, magonjwa yote—ya kimwili, ya kiakili, na ya kihisia-moyo—yataponywa. Hilo laonyeshwa vyema kwa ‘kuponywa kwa mataifa’ kupitia miti hiyo ya ufananisho. Kwa sababu ya maandalizi yatakayotolewa na Kristo pamoja na wale 144,000, “hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24)
-