-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
3, 4. Ni nani “wafanyao maovu juu ya hilo agano,” nao wamekuwa na uhusiano gani na mfalme wa kaskazini?
3 “Na wao wafanyao maovu juu ya hilo agano,” akasema malaika wa Mungu, mfalme wa kaskazini “atawapotosha kwa maneno ya kujipendekeza.” Kisha malaika akasema hivi: “Lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu.
-
-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
4 Wale “wafanyao maovu juu ya hilo agano” waweza tu kuwa viongozi wa Jumuiya ya Wakristo, wanaodai kuwa Wakristo lakini kulingana na matendo yao wanalichafua jina lenyewe la Ukristo. Katika kitabu chake Religion in the Soviet Union, Walter Kolarz asema hivi: “[Wakati wa vita ya ulimwengu ya pili] Serikali ya Sovieti ilijitahidi kuungwa mkono kihalisi na kiadili na Makanisa ili kulinda nchi yao.” Baada ya vita hiyo viongozi wa kanisa walijaribu kudumisha urafiki, ijapokuwa serikali ya mfalme wa kaskazini ilikuwa na sera za kutoamini kuwapo kwa Mungu. Kwa hiyo, Jumuiya ya Wakristo ikawa sehemu ya ulimwengu huu kuliko wakati mwingine wowote—uasi imani wenye kuchukiza machoni pa Yehova.—Yohana 17:16; Yakobo 4:4.
5, 6. “Watu wamjuao Mungu wao” walikuwa nani, na walipatwa na hali gani chini ya mfalme wa kaskazini?
5 Vipi juu ya Wakristo wa kweli—“watu wamjuao Mungu wao” na “wenye hekima”? Ingawa walikuwa “katika ujitiisho kwa mamlaka zilizo kubwa” ifaavyo, Wakristo walioishi chini ya utawala wa mfalme wa kaskazini hawakuwa sehemu ya ulimwengu. (Waroma 13:1; Yohana 18:36) Walikuwa waangalifu kumlipa “Kaisari vitu vya Kaisari,” na kumlimpa “Mungu vitu vya Mungu.” (Mathayo 22:21) Kwa sababu hiyo, uaminifu-maadili wao ulijaribiwa.—2 Timotheo 3:12.
6 Kwa sababu hiyo, Wakristo wa kweli ‘walianguka’ na ‘wakawa hodari.’ Walianguka katika maana ya kwamba walinyanyaswa vikali, hata wengine wakauawa. Lakini walikuwa hodari katika maana ya kwamba walio wengi waliendelea kuwa waaminifu. Waliushinda ulimwengu, kama alivyofanya Yesu. (Yohana 16:33) Isitoshe, hawakuacha kuhubiri, hata ikiwa walifungwa gerezani au kwenye kambi za mateso.
-