-
Mikono Yenu na Iwe na NguvuMnara wa Mlinzi—2006 | Aprili 15
-
-
18. Kulingana na Zekaria sura ya 14, ni mambo gani yatakayotukia wakati ujao?
18 Zekaria alirejelea uharibifu wa Babiloni Mkubwa unaofuatiwa na vita vya Har–Magedoni. Tunasoma hivi: “Itakuwa siku moja inayojulikana kuwa ni ya Yehova. Haitakuwa mchana, wala haitakuwa usiku; na itatukia kwamba wakati wa jioni kutakuwa na nuru.” Naam, siku ya Yehova itakuwa yenye giza kwelikweli, siku isiyopendeza kwa adui zake duniani! Lakini itakuwa siku nzuri na yenye nuru kwa waabudu waaminifu wa Yehova.
-