-
‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
-
-
17. Jambo ambalo Yehova alifanya lilikuwa “kinyume cha asili” jinsi gani?
17 Yehova alifanya jambo ambalo wengi hawakutazamia kabisa. Paulo anaeleza yale yaliyotukia kuwa “kinyume cha asili.” (Rom. 11:24) Hilo lilitukia jinsi gani? Kwa kweli, lingeonekana kuwa jambo lisilo la kawaida, hata lisilo la asili, kupandikiza tawi la mwituni kwenye mti uliopandwa, lakini hivyo ndivyo wakulima fulani walivyofanya katika karne ya kwanza.b Kwa njia hiyohiyo, Yehova alifanya jambo fulani lisilo la kawaida. Kwa maoni ya Wayahudi, Watu wa Mataifa hawangeweza kuzaa matunda yenye kukubalika. Hata hivyo, Yehova aliwafanya watu hao wa mataifa kuwa sehemu ya “taifa” ambalo lilizaa matunda ya Ufalme. (Mt. 21:43) Kuanzia mwaka wa 36 W.K., wakati Kornelio, Mtu wa kwanza wa Mataifa asiyetahiriwa alipogeuzwa imani na kutiwa mafuta, mlango ulifunguliwa kwa watu wasio Wayahudi ambao hawakuwa wametahiriwa kupandikizwa kwenye mzeituni huo wa mfano.—Mdo. 10:44-48.c
18. Wayahudi wa asili walikuwa na nafasi gani baada ya mwaka wa 36 W.K.?
18 Je, hilo linamaanisha kwamba baada ya mwaka wa 36 W.K., Wayahudi wa asili hawakuwa tena na nafasi ya kuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu? Hapana. Paulo anaeleza: “Wao pia [Wayahudi wa asili], ikiwa hawatadumu katika ukosefu wao wa imani, watapandikizwa; kwa maana Mungu anaweza kuwapandikiza tena. Kwa maana ikiwa wewe ulikatwa kutoka kwenye mzeituni ulio wa asili ya mwituni na kupandikizwa kinyume cha asili katika mzeituni wa bustanini, si afadhali zaidi kwamba hawa walio wa asili wapandikizwe katika mzeituni wao wenyewe!”d—Rom. 11:23, 24.
-
-
‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
-
-
d Kiambishi au neno la Kigiriki linalotafsiriwa “bustani” katika andiko la Waroma 11:24 linatokana na neno linalomaanisha “-zuri, bora sana” au “kitu kinachofaana vizuri na makusudi yake.” Kiambishi hicho kinatumiwa hasa kuhusu vitu ambavyo vinatimiza kusudi ambalo vilitengenezwa vitimize.
-