-
“Msimlipe Yeyote Uovu Kwa Uovu”Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
-
-
“Msijilipizie Kisasi Wenyewe”
15. Andiko la Waroma 12:19 linaonyesha sababu gani ya kutolipiza kisasi?
15 Paulo anatoa sababu nyingine nzuri ya kutolipiza kisasi; mwenendo huo unaonyesha kwamba tuna sifa ya kiasi. Anasema hivi: “Wapendwa, msijilipizie kisasi wenyewe bali iachieni nafasi ghadhabu; kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.’” (Waroma 12:19) Mkristo ambaye anajaribu kulipiza kisasi ana kimbelembele. Anajichukulia daraka ambalo ni la Mungu. (Mathayo 7:1) Kwa kuongezea, anapojichukulia mambo mikononi mwake, anaonyesha kwamba hana imani katika uhakikisho huu wa Yehova: “Mimi nitalipa.” Kinyume cha hilo, Wakristo wa kweli wanasadiki kwamba Yehova “atasababisha haki ifanywe kwa ajili ya watu wake waliochaguliwa.” (Luka 18:7, 8; 2 Wathesalonike 1:6-8) Wanaonyesha sifa ya kiasi kwa kumwachia Mungu daraka la kulipiza uovu.—Yeremia 30:23, 24; Waroma 1:18.
-
-
“Msimlipe Yeyote Uovu Kwa Uovu”Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
-
-
Tatu, tunaonyesha sifa ya kiasi kwa kutolipa uovu kwa uovu. Kujilipizia kisasi ni kuwa na kimbelembele, kwa kuwa Yehova anasema: “Kisasi ni changu.” Neno la Mungu linatuonya hivi pia: “Je, kimbelembele kimekuja? Basi aibu itakuja; lakini wenye kiasi wana hekima.” (Methali 11:2) Tunaonyesha sifa ya kiasi tunapomwachia Mungu daraka la kulipiza uovu.
-