-
Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Ndoa Yenye MatatizoMnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
-
-
lakini kwa kweli akiondoka, na akae mseja kama sivyo apatane tena na mume wake; na mume hapaswi kumwacha mke wake
-
-
Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Ndoa Yenye MatatizoMnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
-
-
14, 15. Ni wakati gani kwa kweli mwenzi wa ndoa Mkristo anaweza kufikiria kuondoka, lakini kwa nini ni muhimu asali kuhusu jambo hilo na kulifikiria kwa unyoofu?
14 Ni katika hali gani mke Mkristo anaweza ‘kwa kweli kuondoka’? Wengine wameamua kutengana kwa sababu mwenzi wao anakataa kimakusudi kuandaa mahitaji ya familia. Wengine wametengana kwa sababu mwenzi wao anawatesa sana kimwili au anahatarisha kabisa hali yao ya kiroho wakiwa Wakristo.
15 Kutengana au kutotengana na mwenzi wa ndoa ni uamuzi wa mtu binafsi. Hata hivyo, mwenzi aliyebatizwa anapaswa kusali kuhusu jambo hilo na kulifikiria kwa unyoofu. Kwa mfano, je, mwenzi ambaye si mwamini ndiye ambaye amehatarisha kabisa hali ya kiroho ya mwenzi Mkristo, au je, Mkristo mwenyewe amekuwa akipuuza funzo la Biblia, amekuwa hahudhurii mikutano kwa ukawaida, na hashiriki kwa ukawaida katika huduma?
-