-
‘Tenda Haki’ Unapotembea na MunguMkaribie Yehova
-
-
Linatusihi pia ‘tuvae utu mpya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli.’ (Waefeso 4:24) Uadilifu wa kweli, au haki ya kweli, huchukia jeuri, uovu, na ukosefu wa adili, kwa sababu mambo hayo huchafua mambo matakatifu.—Zaburi 11:5; Waefeso 5:3-5.
-
-
‘Tenda Haki’ Unapotembea na MunguMkaribie Yehova
-
-
6 Si rahisi kwa wanadamu wasiokamilika kufuatia uadilifu. Ni lazima tuvue utu wa zamani pamoja na mazoea yake maovu na kujivika utu mpya. Biblia inasema kwamba utu huo mpya “unafanywa kuwa mpya” kupitia ujuzi sahihi. (Wakolosai 3:9, 10) Maneno ya lugha ya awali yaliyotafsiriwa “-fanywa kuwa mpya” yanaonyesha kwamba kujivika utu mpya ni jambo lenye kuendelea, ambalo linahitaji jitihada kubwa. Hata tukijitahidi kadiri gani kufanya yaliyo mema, nyakati nyingine tunakosea katika mawazo, maneno, au matendo kwa sababu ya hali yetu ya dhambi.—Waroma 7:14-20; Yakobo 3:2.
-