-
Dumisha Hisi Yako ya UharakaMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
Kwa maana kutakuwa na kipindi cha wakati ambapo hawatalivumilia fundisho lenye afya, bali, kwa kupatana na tamaa zao wenyewe, watajikusanyia walimu kwa ajili yao wenyewe ili masikio yao yafurahishwe; nao watageuza masikio yao kutoka kwenye kweli.” (2 Tim. 4:2-4)
-
-
Dumisha Hisi Yako ya UharakaMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
Kwa maana kutakuwa na kipindi cha wakati ambapo hawatalivumilia fundisho lenye afya, bali, kwa kupatana na tamaa zao wenyewe, watajikusanyia walimu kwa ajili yao wenyewe ili masikio yao yafurahishwe; nao watageuza masikio yao kutoka kwenye kweli.” (2 Tim. 4:2-4)
-
-
Dumisha Hisi Yako ya UharakaMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
Ni mafundisho gani ya uwongo ambayo yanafurahisha masikio ya watu leo? Katika maeneo mengi, fundisho la mageuzi limeenezwa kwa bidii kama fundisho la kidini. Ingawa kwa kawaida lugha ya kisayansi inatumiwa ili kueleza fundisho la mageuzi, ni kana kwamba fundisho hilo limekuwa dini ambayo inaathiri maoni ya watu juu ya Mungu na watu wengine. Fundisho lingine ambalo limeenea ni lile la kwamba Mungu hapendezwi nasi; na hivyo, sisi pia hatuhitaji kupendezwa naye. Kwa nini mafundisho hayo yanavutia sana hivi kwamba yanawafanya mamilioni ya watu walale usingizi wa kiroho? Mafundisho yote mawili yanakufanya uamini kwamba ‘Unaweza kufanya jambo lolote unalotaka kwa sababu hutatozwa hesabu.’ Kwa kweli huo ni ujumbe ambao umefurahisha masikio ya watu wengi.—Soma Zaburi 10:4.
6 Lakini kuna njia nyingine ambazo zinatumiwa ili kufurahisha masikio ya watu. Watu fulani ambao bado wanaenda kanisani wanapenda walimu ambao wanawaambia hivi: ‘Hata utende jambo gani, Mungu anakupenda.’ Mapadri na makasisi wanafurahisha masikio ya wengine kwa kuwasadikisha kwamba sherehe, Misa, sikukuu za kidini, na sanamu zinakubaliwa na Mungu. Huenda watu hao wanaoenda kanisani wasitambue kwamba wako katika hali ya hatari. (Zab. 115:4-8)
-