-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ijapokuwa kazi ya kuhubiri haikuwa imetia mizizi, gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 1925, liliripoti: “Vijitabu The Harp of God, The Desirable Government na The World Distress vilikuwa vimetafsiriwa na kuchapishwa katika lugha ya wenyeji . . . Vimesambazwa kwa wingi nao Waalbania wanaikubali kweli kwa shangwe.”
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Pia kitabu The Harp of God (Kinubi cha Mungu) kilisomwa sana, licha ya makosa fulani katika tafsiri. (Kwa mfano, mwanzoni kichwa cha kitabu hicho kilitafsiriwa, The Guitar of God [Gita ya Mungu].) Hata hivyo, kitabu hicho kiliwasaidia Waalbania wengi kujifunza kweli za Biblia na kuimarisha imani yao.
-