-
Ni Nani Atakayeutawala Ulimwengu?Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
UTAWALA WENYE KUDUMU U KARIBU!
36, 37. (a) ‘Mmoja aliye mfano wa mwana wa binadamu’ ni nani, naye alitokea kwenye Mahakama ya kimbingu lini na kwa kusudi gani? (b) Ni nini kilichosimamishwa mwaka wa 1914 W.K.?
36 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama,” akasema Danieli kwa mshangao. “Mmoja aliye mfano wa mwanadamu [“mwana wa binadamu,” NW] akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.” (Danieli 7:13) Alipokuwa duniani, Yesu Kristo alijiita “Mwana wa binadamu,” akionyesha uhusiano wake na wanadamu. (Mathayo 16:13; 25:31) Yesu aliiambia Sanhedrini, au mahakama kuu ya Kiyahudi hivi: “Mtaona Mwana wa binadamu ameketi kwenye mkono wa kuume wa nguvu na akija juu ya mawingu ya mbinguni.” (Mathayo 26:64) Kwa hiyo, katika ono la Danieli, yule ajaye, asiyeonekana kwa macho ya kibinadamu, na kumwendea Yehova Mungu alikuwa Yesu Kristo aliyefufuliwa na kutukuzwa. Hilo lilitukia lini?
37 Mungu amefanya agano na Yesu Kristo kwa ajili ya Ufalme, kama vile tu alivyokuwa amefanya agano na Mfalme Daudi. (2 Samweli 7:11-16; Luka 22:28-30) “Nyakati zilizowekwa rasmi za mataifa” zilipoisha mwaka wa 1914 W.K., Yesu Kristo, akiwa mrithi wa ufalme wa Daudi, alikuwa na haki ya kupokea utawala wa Ufalme. Rekodi ya kiunabii ya Danieli yasema hivi: “Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.” (Danieli 7:14) Kwa hiyo, Ufalme wa Kimesiya ulisimamishwa mbinguni mwaka wa 1914. Hata hivyo, wengine pia wanapewa utawala huo.
-
-
Ni Nani Atakayeutawala Ulimwengu?Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 147]
-