-
Yehova Hutoa Amani na Kweli kwa WingiMnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
-
-
‘Nitakuwa na Wivu kwa Ajili ya Sayuni’
6, 7. Ni katika njia gani Yehova alikuwa ‘mwenye wivu kwa ajili ya Sayuni kwa ghadhabu kuu’?
6 Usemi huo watokea mara ya kwanza kwenye Zekaria 8:2, ambapo twasoma hivi: ‘BWANA wa majeshi asema hivi, Mimi nitakuwa na wivu kwa ajili ya Sayuni, wivu mkuu, nami nitakuwa na wivu kwa ajili yake kwa ghadhabu kuu.’ Ahadi ya Yehova ya kuwa mwenye wivu, kuwa na bidii sana, kwa ajili ya watu wake ilimaanisha kwamba angekuwa macho ili awarudishie amani. Kurudishwa kwa Israeli katika bara lalo na kujengwa upya kwa hekalu kulikuwa uthibitisho wa bidii hiyo.
7 Lakini, vipi juu ya wale ambao walikuwa wamepinga watu wa Yehova? Bidii yake kwa ajili ya watu wake ingetoshana na ‘ghadhabu yake kuu’ juu ya maadui wake. Wayahudi waaminifu walipoabudu kwenye hekalu lililojengwa upya, wangeweza kufikiria yale yaliyopata Babiloni lenye nguvu, ambalo sasa lilikuwa limeanguka. Pia waliweza kufikiria juu ya kushindwa kabisa kwa maadui waliojaribu kuzuia kujengwa upya kwa hekalu. (Ezra 4:1-6; 6:3) Nao waliweza kumshukuru Yehova kwamba alikuwa ametimiza ahadi yake. Bidii yake iliwaletea ushindi!
-
-
Yehova Hutoa Amani na Kweli kwa WingiMnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
-
-
11. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamejionyeshaje kuwa maadui wa watu wa Mungu?
11 Lakini, namna gani juu ya maadui wa Israeli wa Mungu? Bidii ya Yehova kwa ajili ya watu wake yalingana na ghadhabu yake dhidi ya wapinzani. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walileta mkazo mkubwa sana walipojaribu—na kushindwa—kuondoa kabisa kikundi hiki kidogo cha Wakristo wenye kusema kweli. Wakati wa vita ya ulimwengu ya pili, wahudumu wa Jumuiya ya Wakristo waliungana katika jambo moja tu: Katika pande zote mbili zilizokuwa zikipambana, walihimiza serikali ziwakandamize Mashahidi wa Yehova. Hata leo, katika nchi nyingi viongozi wa kidini wanachochea serikali mbalimbali kuwekea vikwazo au kupiga marufuku kazi ya Kikristo ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova.
12, 13. Ghadhabu ya Yehova yaonyeshwaje dhidi ya Jumuiya ya Wakristo?
12 Hilo halijakosa kuonwa na Yehova. Baada ya vita ya ulimwengu ya kwanza, Jumuiya ya Wakristo, pamoja na sehemu iliyobaki ya Babiloni Mkubwa, ilianguka. (Ufunuo 14:8) Uhalisi wa kuanguka kwa Jumuiya ya Wakristo ukaja kuwa jambo la kujulikana kwa wote wakati, kuanzia 1922, mfululizo wa mapigo ya mifano yalipomwagwa, yakifunua peupe hali yake ya kufa kiroho na kuonya juu ya uharibifu wake unaokuja. (Ufunuo 8:7–9:21) Huku kukiwa na uthibitisho kwamba kumwagwa kwa mapigo hayo kwaendelea, hotuba “Mwisho wa Dini Bandia U Karibu” ilitolewa ulimwenguni pote katika Aprili 23, 1995, ikifuatwa na kugawanywa kwa mamia ya mamilioni ya nakala za toleo la kipekee la Habari za Ufalme.
-