-
Yehova Hupendezwa Sana na Utumishi Wako wa Nafsi YoteMnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
-
-
Zawadi “Ghali Sana” ya Mwanamke Mwenye Uthamini
13. (a) Hali zilikuwaje Maria alipokuwa akimwaga mafuta yenye marashi juu ya kichwa na miguu ya Yesu? (b) Thamani ya kimwili ya mafuta ya Maria ilikuwa kiasi gani?
13 Ijumaa jioni, Nisani 8, Yesu alifika Bethania, kijiji kidogo katika mteremko wa mashariki wa Mlima wa Mizeituni, karibu kilometa tatu kutoka Yerusalemu. Yesu alikuwa na rafiki wapendwa katika mji huu—Maria, Martha, na ndugu yao, Lazaro. Labda mara nyingi, Yesu alikuwa amekuwa mgeni nyumbani kwao. Lakini Jumamosi jioni, Yesu na rafiki zake walikuwa wakila mlo-mkuu nyumbani kwa Simoni, aliyekuwa mwenye ukoma hapo zamani ambaye labda aliponywa na Yesu. Yesu alipokuwa akiegama mezani, Maria alifanya kitendo cha unyenyekevu kilichoonyesha upendo wake wenye kina kwa mwanamume ambaye alikuwa amemfufua ndugu yake. Aliivunja ili kufungua chupa iliyokuwa na mafuta yenye marashi, “ghali sana.” Ghali, kwelikweli! Yalikuwa na thamani ya dinari 300, kiasi kinacholingana na mshahara wa mwaka mzima. Aliyamwaga mafuta haya yenye marashi kichwani mwa Yesu na juu ya miguu yake. Hata alipangusa miguu yake mpaka ikakauka kwa nywele zake.—Marko 14:3; Luka 10:38-42; Yohana 11:38-44; 12:1-3.
14. (a) Wanafunzi waliitikiaje tendo la Maria? (b) Yesu alimteteaje Maria?
14 Wanafunzi walihisi uchungu! ‘Kwa nini upotevu huu?’ wakauliza. Yudasi, akiwa na tamaa yake ya kuiba akisingizia kudokeza uhitaji wa kusaidia wenye uhitaji, alisema: “Kwa nini mafuta haya yenye marashi hayakuuzwa kwa dinari mia tatu na kupewa kwa maskini?” Maria alinyamaza. Hata hivyo, Yesu aliwaambia wanafunzi hivi: “Mwacheni. Kwa nini mwajaribu kumsumbua? Alifanya kitendo bora [namna ya ka·losʹ] kunielekea mimi. . . . Alifanya lile ambalo angeweza; alijitwalia daraka kimbele kutia mafuta yenye marashi juu ya mwili wangu kwa kufikiria maziko. Kwa kweli nawaambia nyinyi, Kokote ambako habari njema yahubiriwa katika ulimwengu wote, alilofanya mwanamke huyu hakika litasimuliwa pia kuwa ukumbuko juu yake.” Lazima iwe uchangamfu wa maneno ya Yesu uliutuliza moyo wa Maria jinsi gani!—Marko 14:4-9; Yohana 12:4-8.
15. Kwa nini Yesu alichochewa sana na lile ambalo Maria alifanya, nasi twajifunza nini kwa njia hiyo kuhusu utumishi wa nafsi yote?
15 Yesu alichochewa sana na lile ambalo Maria alikuwa amefanya. Kwa kukadiria kwake, alikuwa amefanya jambo lenye kustahiki sifa. Jambo la maana kwa Yesu halikuwa thamani ya kimwili ya zawadi bali uhakika wa kwamba “alifanya lile ambalo angeweza.” Alitumia kwa manufaa fursa hiyo, akatoa kile alichoweza kutoa. Tafsiri nyingine zimetafsiri maneno haya, “Amefanya yote ambayo angeweza,” au, “Amefanya lililokuwa katika uwezo wake kufanya.” (An American Translation; The Jerusalem Bible) Kutoa kwa Maria kulikuwa kwa nafsi yote kwa sababu alitoa yaliyo bora zaidi. Hiyo ndiyo maana ya utumishi wa nafsi yote.
-
-
Yehova Hupendezwa Sana na Utumishi Wako wa Nafsi YoteMnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
-
-
18. Twajifunza nini kutokana na kushughulika kwa Yesu na hao wanawake wawili?
18 Kutokana na kushughulika kwa Yesu na wanawake hawa wawili, twajifunza masomo fulani yenye kuchangamsha moyo juu ya jinsi Yehova anavyoona utumishi wa nafsi yote. (Yohana 5:19) Yesu hakumlinganisha mjane na Maria. Alithamini sarafu mbili za mjane kama vile alivyothamini mafuta “ghali sana” ya Maria. Kwa kuwa kila mwanamke alitoa zawadi yake iliyo bora zaidi, machoni pa Mungu zawadi zote mbili zilikuwa zenye thamani. Kwa hiyo ukijawa na hisia za kutofaa kitu kwa sababu huwezi kufanya yote unayotaka kufanya katika kumtumikia Mungu, usikate tumaini. Yehova anapendezwa kukubali yote uwezayo kutoa. Kumbuka, Yehova “huutazama moyo,” kwa hiyo yeye ajua kikamili tamaa za moyo wako.—1 Samweli 16:7.
-