-
Apokalipsi—Je, Tuiogope Au Tuitumainie?Mnara wa Mlinzi—1999 | Desemba 1
-
-
Tumaini Zuri Ajabu la Apokalipsi Lingali Lipo!
Mashahidi wa Yehova husadiki kwamba ahadi nzuri ajabu zinazohusu Milenia zitatimizwa. Alipohojiwa kwenye programu ya televisheni ya Ufaransa juu ya habari isemayo “Mwaka wa 2000: Woga wa Apokalipsi,” mwanahistoria Mfaransa Jean Delumeau alisema hivi: “Mashahidi wa Yehova wanafuata kabisa fundisho la milenia, kwa sababu wao husema kwamba karibuni . . . tutaingia katika kipindi cha miaka 1,000 chenye furaha japo kupitia magumu.”
Hilo ndilo jambo ambalo mtume Yohana aliona na kufafanua katika kitabu chake Apokalipsi, au Ufunuo. Aliandika: “Nikaona mbingu mpya na dunia mpya . . . Ndipo nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha ufalme ikisema: ‘Tazama! Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa vikundi vya watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kabisa kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.’”—Ufunuo 21:1, 3, 4.
Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi ya ulimwenguni pote ya kufundisha watu Biblia ili kuwawezesha watu wengi iwezekanavyo wawe na tumaini hilo. Watafurahi kukusaidia ujifunze mengi zaidi kulihusu.
-
-
“Taarifa za Mteremo” Kutoka Kwenye ApokalipsiMnara wa Mlinzi—1999 | Desemba 1
-
-
1. Ingawa Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba kitabu cha Apokalipsi kimepuliziwa, kwa nini wao si “madhehebu ya kutabiri maangamizi tu”?
TOFAUTI na mashtaka wanayofanyiwa, Mashahidi wa Yehova si “madhehebu ya kutabiri maangamizi tu” wala “madhehebu inayotabiri uharibifu.” Hata hivyo, wao hukubali Apokalipsi, au kitabu cha Ufunuo, kuwa sehemu ya Neno la Mungu lililopuliziwa. Ni kweli kwamba kitabu cha Ufunuo kina ujumbe wenye hukumu dhidi ya waovu. Lakini wanapohubiri waziwazi watumishi wa Mungu hukazia hasa tumaini zuri ajabu linalotajwa katika Biblia, kutia ndani tumaini linalopatikana katika Apokalipsi, au Ufunuo. Hivyo, wao hawaongezei wala hawaondoi neno lolote kwenye maneno ya unabii yanayopatikana humo.—Ufunuo 22:18, 19.
Matangazo ya Taarifa za Mteremo
2. Mashahidi wa Yehova hutumia maandiko gani katika kazi yao ya kuhubiri?
2 Andiko ambalo hutajwa mara nyingi kuwa msingi wa huduma ya waziwazi ya Mashahidi wa Yehova ni taarifa hii ya Yesu: “Habari njema hii ya ufalme itatangazwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14, kielezi-chini katika New World Translation of the Holy Scriptures—With References) “Habari njema hii ya ufalme” ni nini? Mashahidi wengi hujibu kwa kunukuu mistari ya Ufunuo sura ya 20 na 21 inayorejezea ule Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo na serikali yake ya Ufalme na jamii ya wanadamu, ambamo kifo, maombolezo, na maumivu ‘hazitakuwapo tena kamwe.’—Ufunuo 20:6; 21:1, 4.
3. Huduma ya waziwazi ya Mashahidi wa Yehova yalingana na utume gani?
3 Kwa kuwa Mashahidi wa Yehova ni watangazaji wa taarifa hizi za mteremo, kwa kweli wao ni wasemaji wa mjumbe wa kimbingu wa mfano ambaye utume wake unatajwa pia katika Ufunuo. “Nikaona malaika mwingine akiruka katika mbingu ya kati, naye alikuwa na habari njema idumuyo milele ili aitangaze kuwa taarifa za mteremo kwa wale wakaao juu ya dunia, na kwa kila taifa na kabila na lugha na watu.” (Ufunuo 14:6) Hiyo “habari njema idumuyo milele” yatia ndani tangazo la kwamba “ufalme [au, utawala] wa ulimwengu” umekuwa “ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake” na kwamba “wakati [wa Yehova] uliowekwa rasmi” umefika wa “kuwaleta kwenye uangamizi wale wanaoiangamiza dunia.” (Ufunuo 11:15, 17, 18) Je, kweli hiyo si habari njema?
-