Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ule Uasi-imani Mkubwa Wasitawi
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mara watu wenye mawazo ya kufuata falsafa walipokuja kuwa Wakristo, haikuchukua muda mrefu kabla ya falsafa ya Kigiriki na ule uitwao eti “Ukristo” kuungana kwa njia isiyotenganika.

      Tokeo la muungano huo ni kwamba, mafundisho ya kipagani kama vile Utatu na kutokufa kwa nafsi yalipenyeza polepole yakaingia katika Ukristo uliochafuliwa. Hata hivyo, mafundisho hayo yarudi nyuma mbali sana kupita wanafalsafa Wagiriki. Kwa kweli Wagiriki waliyapata kutokana na tamaduni za zamani zaidi, kwa maana kuna uthibitisho wa kwamba mafundisho hayo yalikuwa katika dini za kale za Kimisri na Kibabiloni.

  • Ule Uasi-imani Mkubwa Wasitawi
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mwanafalsafa Mgiriki Plato (aliyezaliwa kama 428 K.W.K.) hakuwa na njia ya kujua kwamba hatimaye mafundisho yake yangepata njia ya kuingia ndani ya Ukristo ulioasi imani. Mambo makuu ambayo Plato aliuchangia “Ukristo” yalihusu mafundisho ya Utatu na kutokufa kwa nafsi.

      Mawazo ya Plato juu ya Mungu na asili yalikuwa na uvutano juu ya fundisho la Utatu la Jumuiya ya Wakristo. Chaeleza hivi “Nouveau Dictionnaire Universel”: “Utatu wa Kiplato, wenyewe ukiwa ni mpango mpya tu wa utatu-utatu mwingi wa kale zaidi wenye kurudi nyuma kwenye watu wa mapema kabisa, huonekana kuwa ni utatu wa maelezo ya akili ya kifalsafa ya sifa zilizozaa nyutu tatu au watu wa kimungu wanaofundishwa na makanisa ya Kikristo. . . . Wazo hili la mwanafalsafa Mgiriki la utatu wa kimungu . . . laweza kupatikana katika dini zote za kale [za kipagani].”—Buku la 2, ukurasa 1467.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki