Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya Bwana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 4. (a) Ni tangu lini watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914? (b) 1914 ungetia alama ya mwisho wa kipindi gani cha wakati?

      4 Kuanzia miaka ya katikati ya 1870 watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914 nayo yangeonyesha mwisho wa Majira ya Mataifa. Hiki ndicho kipindi cha “nyakati saba” (miaka 2,520) kikianza na kupinduliwa kwa ufalme wa Kidaudi katika Yerusalemu katika 607 K.W.K. hadi kuketishwa kwa Yesu juu ya kiti cha ufalme katika Yerusalemu la kimbingu katika 1914 W.K.—Danieli 4:24, 25; Luka 21:24.b

  • Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya Bwana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 105]

      1914 Ulitangulia Kuonwa

      “Ilikuwa katika K.K. 606, kwamba ufalme wa Mungu ulikwisha, taji liliondolewa, na dunia yote ikapewa Wasio Wayahudi. Miaka 2520 kutoka K.K. 606, itakwisha katika M.B. 1914.”f—The Three Worlds, kilichotangazwa 1877, ukurasa 83.

      “Ithibati ya Biblia ni wazi na thabiti kwamba ‘Majira ya Mataifa’ ni kipindi cha miaka 2520, kutoka K.K. 606 kufika na kutia ndani M.B. 1914”—Studies in the Scriptures, Buku 2, kilichoandikwa na C. T. Russell na kikatangazwa 1889, ukurasa 79.

      Charles Taze Russell na Wanafunzi wa Biblia wenzake waling’amua miongo kadhaa mapema zaidi kwamba 1914 ungeonyesha mwisho wa Majira ya Mataifa, au nyakati zilizowekwa za mataifa. (Luka 21:24) Ingawa katika siku hizo za mapema wao hawakuelewa kikamili hii ingemaanisha nini, wao walisadikishwa kwamba 1914 ingekuwa tarehe ya mabadiliko katika historia ya ulimwengu, nao walikuwa sahihi. Angalia dondoo hili linalofuata la nyusipepa:

      “Ule mfyatuko wa vita wenye kuogopesha katika Ulaya umetimiza unabii usio wa kawaida. Kwa robo ya karne iliyopita, kupitia wahubiri na kupitia magazeti, wale ‘Wanafunzi wa Biblia,’ wanaojulikana vizuri zaidi kuwa ‘Wanamapambazuko wa Mileani,’ wamekuwa wakitangazia ulimwengu kwamba ile Siku ya Hasira-Kisasi iliyotolewa unabii na Biblia ingepambazuka katika 1914. ‘Lindeni kwa ajili ya 1914!’ kimekuwa ndicho kilio cha mamia ya waevanjeli wasafirio.”—The World, nyusipepa moja ya New York, Agosti 30, 1914.

      [Maelezo ya Chini]

      f Kwa uongozi wa kimungu, hao Wanafunzi wa Biblia hawakuwa wameng’amua kwamba hakukuwa na mwaka sufuri katikati ya “K.K.” na “M.B.” Baadaye, wakati utafiti ulipofanya ihitajiwe kabisa kurekebisha K.K. 606 kuwa 607 K.W.K., ule mwaka sufuri uliondolewa pia, hivi kwamba ule utabiri ukawa sahihi kwenye “M.B. 1914.”—Ona “The Truth Shall Make You Free,” kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova mwaka wa 1943, ukurasa 239.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki