-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Unabii Mbalimbali Unaohusu Wakati na Kuwapo kwa Bwana
Asubuhi moja katika Januari 1876, Russell mwenye umri wa miaka 23 alipokea nakala ya jarida la kidini linaloitwa Herald of the Morning. Kutokana na picha katika jalada, yeye angeweza kuona kwamba lilihusiana na Uadventisti. Mhariri, Nelson H. Barbour, wa Rochester, New York, aliamini kwamba lengo la kurudi kwa Kristo si kuharibu familia za dunia bali kuzibariki na kwamba kuja kwake kungekuwa si katika mwili bali akiwa roho. Aa! hilo lilipatana na yale ambayo Russell na washirika wake katika Allegheny walikuwa wameamini kwa muda fulani!b Ingawa hivyo, ajabu ni kwamba Barbour aliamini kutokana na unabii mbalimbali unaohusu wakati wa Kibiblia kwamba Kristo alikuwa tayari yupo (bila kuonekana) na kwamba wakati ulikuwa umefika wa kufanya kazi ya mavuno ya kukusanya “ngano” (Wakristo wa kweli waliojumuika kuwa jamii ya Ufalme).—Mt., sura 13.
Russell alikuwa ameepuka unabii mbalimbali wa Kibiblia unaohusu wakati. Lakini, sasa, yeye alijiuliza: “Je, ingeweza kuwa kwamba unabii mbalimbali unaohusu wakati ambao nilikuwa nimepuuza kwa muda mrefu sana, kwa sababu ya kutumiwa vibaya na Waadventisti, ulikuwa kwa kweli umekusudiwa uonyeshe wakati ambao Bwana angekuwapo bila kuonekana ili kusimamisha Ufalme wake?” Akiwa na kile kiu chake kisichotoshelezeka cha kweli ya Kimaandiko, ilikuwa sharti Russell ajifunze zaidi. Hivyo alipanga kukutana na Barbour katika Philadelphia. Mkutano huo ulithibitisha maafikiano yao juu ya mafundisho kadhaa ya Biblia na kuandaa fursa kwao wajadiliane. “Tulipokutana mara ya kwanza,” Russell akataarifu baadaye, “alikuwa na mengi ya kujifunza kutoka kwangu juu ya ujalivu wa rudisho unaotegemea utoshelevu wa fidia iliyotolewa kwa ajili ya wote, kama vile mimi nilivyokuwa na mengi ya kujifunza kutoka kwake juu ya wakati.” Barbour alifaulu kumsadikisha Russell kwamba kuwapo kusikoonekana kwa Kristo kulikuwa kumeanza katika 1874.c
‘Aazimia Kufanya Kampeni Yenye Juhudi kwa Ajili ya Kweli’
C. T. Russell alikuwa mtu wa masadikisho hakika. Akiwa amesadikishwa kwamba kuwapo kusikoonekana kwa Kristo kulikuwa kumeanza, aliazimia kupiga mbiu ya jambo hilo kwa wengine. Baadaye alisema hivi: “Kujua uhakika wa kwamba tayari tulikuwa katika kipindi cha mavuno kulinipa msukumo wa kueneza Kweli ambao sikuwa nimepata kuwa nao hapo awali. Kwa hiyo niliazimia kufanya kampeni yenye juhudi kwa ajili ya Kweli.” Sasa Russell aliamua kupunguza shughuli zake za kibiashara ili ajitoe mwenyewe afanye kazi ya kuhubiri.
Ili kupinga maoni yoyote yenye kosa kuhusu kurudi kwa Bwana, Russell aliandika kijitabu The Object and Manner of Our Lord’s Return. Kilitangazwa katika 1877. Mwaka huohuo Barbour na Russell walitangaza kwa kushirikiana kitabu Three Worlds, and the Harvest of This World. Kitabu hiki chenye kurasa 196 kilizungumza habari za rudisho na unabii mbalimbaliunaohusu wakati wa Kibiblia. Ingawa kila habari ilikuwa imezungumzwa na wengine awali, katika maoni ya Russell kitabu hiki kilikuwa ndicho “cha kwanza kuunganisha hilo wazo la rudisho na unabii unaohusu wakati.” Kilitoa maoni ya kwamba kuwapo kusikoonekana kwa Yesu Kristo kulianza tarehe ya vuli ya mwaka 1874.
Russell alipokuwa akisafiri na kuhubiri, ikawa wazi kwake kwamba kitu fulani zaidi kilihitajiwa ili kuendeleza mbegu za kweli alizokuwa akipanda zikiwa hai na zimetiliwa maji. Jawabu lilikuwa nini? “Jarida la kila mwezi,” akasema Russell. Hivyo yeye na Barbour waliamua kufufua utangazaji wa jarida Herald, lililokuwa limeacha kuchapwa kwa sababu ya maandikisho kufutwa na fedha kumalizika. Russell alichanga fedha zake mwenyewe ili kulifufua hilo jarida, akiwa mmoja wa wahariri washirika walo.
Yote yalienda sawasawa kwa kitambo—yaani, mpaka 1878.
Russell Aachana na Barbour
Katika toleo la Agosti 1878 la Herald of the Morning, mlitokea makala iliyoandikwa na Barbour ambayo ilikana thamani yenye kubadilishana na kifo cha Kristo. Russell, ambaye alikuwa mchanga kuliko Barbour kwa miaka karibu 30, angeweza kuona kwamba kwa kweli, huko kulikuwa ni kukana sehemu yenye maana ya fundisho la fidia. Hivyo katika toleo lililofuata (Septemba 1878), Russell, katika makala moja yenye kichwa “Kule Kulipia,” alitetea fidia na kupinga taarifa za Barbour. Ubishi huo uliendelea katika kurasa za jarida hilo kwa miezi michache iliyofuata. Hatimaye, Russell aliamua kujiondoa katika ushirika na Bw. Barbour akaacha kuendelea kulitegemeza Herald kifedha.
Ingawa hivyo, C. T. Russell, alihisi kwamba kujiondoa kwenye Herald hakukutosha; fundisho la fidia lazima litetewe na lazima mbiu ipigwe juu ya kuwapo kwa Kristo. Kwa hiyo, katika Julai 1879, Russell alianza kutangaza Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence.d Russell alikuwa ndiye mhariri na mtangazaji, kukiwa na wengine watano ambao hapo kwanza waliorodheshwa kuwa wachangaji wa makala kwenye safu zalo. Toleo la kwanza lilikuwa na nakala 6,000 zilizochapwa. Kufikia 1914 chapa ya kila toleo ilikuwa nakala kama 50,000.
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 48]
“Nakuachia ‘Herald’”
Katika masika ya 1879, C. T. Russell aliacha kabisa kutegemeza gazeti “Herald of the Morning,” ambalo alikuwa ameshiriki kulitangaza pamoja na N. H. Barbour. Katika barua aliyomwandikia Barbour yenye tarehe ya Mei 3, 1879, Russell alifafanua sababu yake: “Kumezuka tofauti ya maoni kati yetu kwa habari ya fundisho la neno la Baba yetu [kuhusu thamani yenye kubadilisha ya fidia] na ingawa nakupa sifa kwa weupe wote wa moyo na unyoofu katika maoni yako, ambayo nadai mwenyewe maoni yaliyo kinyume, hata hivyo lazima niongozwe na uelewevu wangu mwenyewe wa neno la Baba yetu, na kwa sababu hiyo nakufikiria wewe kuwa unakosea. . . . Mambo yenye kuleta tofauti yaonekana kwangu kuwa ya msingi sana na ya maana sana hivi kwamba ushirika kamili na sikitiko kama lile lipaswalo kuwamo miongoni mwa watangazaji na wahariri wa jarida au gazeti, haupo tena kati yangu nawe, na kwa sababu ndivyo ilivyo, mimi nahisi kwamba uhusiano wetu wapaswa kukoma.”
Katika barua ya kufuatia ya tarehe ya Mei 22, 1879, Russell aliandika hivi: “Sasa nakuachia ‘Herald.’ Najiondoa nisihusiane nalo kabisa, nisiulize chochote kutoka kwako . . . Tafadhali toa tangazo katika nambari ifuatayo ya ‘Herald’ juu ya kujiondoa huko na uondoe jina langu.” Kuanzia toleo la Juni 1879, jina la Russell halikutokea tena akiwa mhariri-msaidizi wa “Herald.”
Barbour aliendelea kutangaza “Herald” mpaka 1903, wakati, kulingana na maandishi yapatikanayo ya maktaba, lilipokoma kuchapishwa. Barbour alikufa miaka michache baadaye, katika 1906.
[Picha]
Nelson H. Barbour
-