Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia
    Amkeni!—2007 | Novemba
    • Kunakili Kulihifadhi Maandishi

      Waisraeli ambao ndio watunzaji wa maandishi ya Biblia ya mapema, walihifadhi kwa uangalifu vitabu vya kukunja vya awali na wakatoa nakala nyingi sana. Kwa mfano, wafalme wa Israeli waliambiwa waandike “nakala ya sheria hii kutoka katika ile iliyo mkononi mwa makuhani Walawi.”—Kumbukumbu la Torati 17:18.

      Waisraeli wengi walipenda kusoma Maandiko na waliyatambua kuwa Neno la Mungu. Hivyo, kunakili maandishi hayo kulifanywa kwa uangalifu mkubwa sana na waandikaji waliokuwa na uzoefu wa hali ya juu. Ezra, mwandikaji ambaye alimwogopa Mungu, anatajwa kuwa “mwandikaji stadi katika sheria ya Musa, ambayo Yehova Mungu wa Israeli alikuwa ametoa.” (Ezra 7:6) Wamasora ambao walinakili Maandiko ya Kiebrania, au “Agano la Kale,” kati ya karne ya sita na ya kumi W.K., walihesabu hata herufi katika maandishi hayo ili wasikosee. Kunakili huko kwa uangalifu kulisaidia kuhakikisha maandishi yalikuwa sahihi na kuokoka kwa Biblia licha ya jitihada kubwa zilizofanywa na maadui ili kuiangamiza.

  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia
    Amkeni!—2007 | Novemba
    • Muda mfupi baada ya waandikaji wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, au “Agano Jipya,” kumaliza kazi yao, nakala za barua zao zilizoongozwa na roho, unabii, na masimulizi ya kihistoria zilienea. Kwa mfano, Yohana aliandika Injili yake huko Efeso au karibu na jiji hilo. Hata hivyo, kipande cha Injili hiyo, ambacho wataalamu wanasema ni sehemu ya nakala iliyoandikwa miaka isiyozidi 50 tangu alipoandika simulizi lake, kilipatikana mamia ya kilomita nchini Misri. Ugunduzi huo ulionyesha kwamba Wakristo katika maeneo ya mbali walikuwa na nakala za maandishi yaliyoongozwa na roho yaliyokuwa yametoka tu kuandikwa.

  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia
    Amkeni!—2007 | Novemba
    • Ingawa hakuna hati za Biblia za awali ambazo zimewahi kupatikana, maelfu ya nakala zilizoandikwa kwa mkono za Biblia nzima au sehemu yake zimeokoka hadi leo. Nyingine kati ya hizo ni za zamani sana. Je, ujumbe ulio katika maandishi ya awali ulibadilika uliponakiliwa? Msomi W. H. Green alisema hivi kuhusu Maandiko ya Kiebrania: “Tunaweza kusema kwamba hakuna maandishi mengine ya zamani ambayo yametufikia yakiwa sahihi kadiri hiyo.” Kuhusu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, mmoja wa wataalamu wakuu wa hati za Biblia, Bwana Frederic Kenyon, aliandika hivi: ‘Tofauti kati ya tarehe za maandishi ya kwanza na tarehe ya uthibitisho wa kale zaidi uliopo leo ni ndogo sana hivi kwamba tofauti hiyo haina maana, na kwa hiyo sasa hakuna msingi wa kuwa na shaka kwamba Maandiko hayakutufikia yakiwa jinsi yalivyoandikwa. Uasilia na uaminifu wa ujumla wa vitabu vya Agano Jipya waweza kuonwa kuwa hatimaye umethibitishwa.’ Pia alisema hivi: “Si kusisitiza mno kusema kwamba kwa msingi maandishi ya Biblia ni hakika. . . . Haiwezi kusemwa hivyo kuhusu kitabu kingine chochote cha kale katika ulimwengu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki