-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Yule mwingine, George Storrs alikuwa mtangazaji wa gazeti Bible Examiner, katika Brooklyn, New York. Storrs, ambaye alizaliwa Desemba 13, 1796, alikuwa amechochewa mwanzoni kuchunguza yale ambayo Biblia ilisema juu ya hali ya wafu kama tokeo la kusoma jambo fulani lililokuwa limetangazwa (ingawa wakati huo bila kujitambulisha jina) na mwanafunzi wa Biblia aliye mwangalifu Henry Grew wa Philadelphia, Pennsylvania. Storrs alipata kuwa mteteaji mwenye bidii wa kile kilichoitwa kutokufa kwenye masharti—fundisho la kwamba nafsi ni yenye kufa na kwamba kutokufa ni zawadi ambayo ingefikiwa na Wakristo waaminifu. Yeye alitoa sababu pia kwamba kwa kuwa waovu hawana hali ya kutokufa, hakuna mateso ya milele. Storrs alisafiri sana, akitoa mihadhara juu ya habari ya kwamba waovu hawana hali ya kutokufa. Miongoni mwa vichapo vyake vilivyotangazwa mlikuwamo Six Sermons, ambacho hatimaye kilifikia mwenezo wa nakala 200,000. Bila shaka, maoni yenye nguvu yenye msingi wa Biblia ya Storrs juu ya kufa kwa nafsi pamoja na kulipia na rudisho (kurudishwa kwa kilichopotezwa kwa sababu ya dhambi ya Adamu; Mdo. 3:21) yalikuwa na uvutano mzuri wenye nguvu kwa kijana Charles T. Russell.
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 46]
George Storrs—“Rafiki na Ndugu”
C. T. Russell alijihisi kuwa na deni kwa George Storrs, ambaye alikuwa na umri mkubwa kuliko wake kwa miaka 56. Russell alikuwa amejifunza mengi kutoka kwa Storrs juu ya kufa kwa nafsi. Kwa hiyo wakati Storrs alipolala akiwa mgonjwa mahututi mwishoni-mwishoni mwa 1879, Russell alijitolea kuchapisha katika “Watch Tower” taarifa juu ya hali ya Storrs. “Ndugu yetu,” akaandika Russell, “ambaye amekuwa mhariri wa ‘The Bible Examiner’ kwa muda mrefu sana ajulikana kwa wengi zaidi kati ya wasomaji wetu; pia kwamba yeye amelazimishwa na ugonjwa mahututi asiendeleze gazeti lake.” Kwa kadirio la Russell, Storrs alikuwa na “sababu nyingi za kumshukuru Mungu kwa kuwa na pendeleo la kutumia maisha marefu sana na ya kujitakasa sana kwa Bwana-Mkubwa.” Storrs alikufa katika Desemba 28, 1879, akiwa na umri wa miaka 83. Tangazo la kifo chake lilitokea katika toleo la Februari 1880 la “Watch Tower,” ambalo lilisema: “Twaomboleza kumpoteza rafiki na ndugu katika Kristo hata hivyo, ‘si kama wale wasio na tumaini.’”
[Picha]
George Storrs
-