-
Hicho Kitabu Kiliokokaje?Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
-
-
Kuhifadhiwa na Wanakiliji Waangalifu Sana
Upesi baada ya maandishi ya awali kuandikwa, nakala zilizoandikwa kwa mkono zilianza kutokezwa. Kwa kweli kunakili Maandiko kulipata kuwa kazi ya kuajiriwa katika Israeli la kale. (Ezra 7:6; Zaburi 45:1) Hata hivyo, nakala hizo pia zilirekodiwa kwenye vifaa viwezavyo kuharibika. Hatimaye nakala nyingine zilizoandikwa kwa mkono zikahitaji kuchukua mahali pa nakala hizo. Maandishi ya awali yalipotoweka, nakala hizi zikawa msingi wa kufanyiza hati za wakati ujao. Kunakili nakala kulikuwa utaratibu ulioendelea kwa karne nyingi. Karne zilipopita, je, makosa ya wanakiliji yalibadili sana maandishi ya Biblia? Uthibitisho wasema la.
Wanakiliji wenye kuajiriwa walikuwa wenye kujitoa sana. Waliyastahi sana maneno waliyoyanakili. Pia walikuwa waangalifu sana. Neno la Kiebrania lifasiriwalo “mnakiliji” ni so·pherʹ, inayorejezea kuhesabu na kurekodi. Ili kutolea kielezi usahihi wa wanakiliji, fikiria Wamasora.a Kuhusu wao, msomi Thomas Hartwell Horne afafanua hivi: “Wao . . . walihesabu ni ipi iliyo herufi ya katikati ya Pentateuki [vitabu vitano vya kwanza vya Biblia], ni kipi kishazi cha katikati cha kila kitabu, na ni mara ngapi kila herufi ya alfabeti [ya Kiebrania] hutokea katika Maandiko yote ya Kiebrania.”3
Hivyo, wanakiliji wastadi walitumia njia kadhaa za kuchunguza kutoka pande mbalimbali. Ili kuepuka kuacha herufi hata moja katika maandishi ya Biblia, walifikia hatua ya kuhesabu si maneno tu yaliyonakiliwa bali pia na herufi. Fikiria ule uangalifu mwingi uliohusika katika hilo: Yaripotiwa kwamba walihesabu herufi mojamoja 815,140 katika Maandiko ya Kiebrania!4 Jitihada hizo nyingi zilihakikisha usahihi wa kadiri ya juu.
Hata hivyo, wanakiliji hawakuwa wasioweza kukosea. Je, kuna uthibitisho wowote wa kwamba, zijapokuwa karne kadhaa za kunakili upya, maandishi ya Biblia yameokoka katika namna ya kutegemeka?
-
-
Hicho Kitabu Kiliokokaje?Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
-
-
a Wamasora (jina limaanishalo “Mabwana-Wakubwa wa Desturi”) walikuwa wanakiliji wa Maandiko ya Kiebrania walioishi kati ya karne ya sita na kumi W.K. Nakala za hati walizotokeza zinarejezewa kuwa maandishi ya Kimasora.2
-