-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mwishoni mwa Desemba 1917 na mapema katika 1918, Wanafunzi wa Biblia katika Marekani na Kanada pia walianza kugawanya nakala 10,000,000 za ujumbe wenye kuchoma katika trakti The Bible Students Monthly. Trakti hiyo ya kurasa nne yenye ukubwa wa kiasi ilikuwa na kichwa “Kuanguka kwa Babiloni,” na ilikuwa na kichwa kidogo “Sababu Kwa Nini Ni Lazima Jumuiya ya Wakristo Iteseke Sasa—Tokeo la Mwisho.” Ilitambulisha matengenezo ya kidini ya Katoliki na Protestanti yakiwa pamoja kuwa Babiloni ya kisasa, ambayo lazima ianguke hivi karibuni. Katika kuunga mkono yale yaliyosemwa, ilitokeza tena kutoka kitabu The Finished Mystery mafafanuzi juu ya unabii mbalimbali unaoonyesha hukumu ya kimungu dhidi ya “Babiloni wa Kifumbo.” Kwenye ukurasa wa nyuma kulikuwa na katuni iliyochorwa kuonyesha ukuta ukiporomoka. Mawe makubwa kutoka kwenye ukuta huo yalikuwa na vibandiko kama vile “Fundisho la Utatu (‘3 X 1 = 1’),” “Kutokufa kwa Nafsi,” “Nadharia ya Mateso ya Milele,” “Uprotestanti—mafundisho, makasisi, n.k.,” “Uroma—mapapa, makadinali, n.k., n.k.”—na mawe hayo yote yalikuwa yakianguka.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 648]
Makasisi walighadhibika wakati nakala 10,000,000 za trakti hii zilipogawanywa zikifunua mafundisho na mazoea yao kwa maoni ya Neno la Mungu
-