-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Huko Sarajevo, programu ingeweza kufanyiwa tu kwenye makutano ya barabara ambapo wavamizi walikuwa wakiwashambulia watu kwa risasi. Akina ndugu walipofika salama kwenye kusanyiko, walikabili tatizo la kupata mahali pa ubatizo na njia ya kuhifadhi maji, ambayo yalipatikana kwa shida. Ili kuhakikisha kwamba kuna maji ya kutosha kwa ajili ya ubatizo, wale wanaotaka kubatizwa waliambiwa wapange foleni kulingana na ukubwa wao, nao wakabatizwa kuanzia yule mdogo zaidi mpaka yule mkubwa zaidi!
Ilikuwa siku yenye furaha kama nini kwa ndugu na dada zetu! Hawakuruhusu matukio yoyote yenye kuogopesha yawanyang’anye shangwe yao kubwa ya kuabudu pamoja. Leo, kuna makutaniko matatu imara katika jiji la Sarajevo.
-
-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Sasa makusanyiko yanafanywa kwa amani katika jiji la Sarajevo, ambako ndugu zetu walishambuliwa mara nyingi na wavamizi wenye kufyatua risasi miaka 10 tu iliyopita.
-