Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Huko Zenica, akina ndugu walipata mahali pazuri pa kukutania, lakini walishindwa kupata kidimbwi cha ubatizo. Mwishowe, baada ya jitihada nyingi, walipata pipa ambalo lingeweza kutumiwa. Lakini tatizo ni kwamba pipa hilo lilikuwa linanuka, kwa kuwa zamani lilitumiwa kuwekea samaki! Hata hivyo, waliotaka kubatizwa ambao walikuwa wameukubali mwaliko wa Yesu wa kuwa “wavuvi wa watu,” hawakuogopa. (Mt. 4:19) Herbert Frenzel, ambaye sasa ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kroatia, alikuwepo ili kutoa hotuba ya ubatizo. Anaripoti hivi: “Wale waliotaka kubatizwa walikuwa wamesubiri kwa muda mrefu sana ili wabatizwe hivi kwamba hakuna jambo ambalo lingewazuia! Baada ya kubatizwa walihisi ni kana kwamba wamepata ushindi!” Leo, kuna kutaniko lenye bidii lenye wahubiri 68 huko Zenica.

  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 204]

      Ubatizo katika pipa la samaki huko Zenica, 1994

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki