-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kuwapa Damu Wanywe
6. Hutukia nini wakati bakuli la tatu linapomiminwa, na ni maneno gani yanayosikiwa kutoka kwa malaika na kutoka madhabahu?
6 Bakuli la tatu la kasirani ya Mungu kama mpigo wa tatu wa tarumbeta, huathiri machimbuko ya maji matamu. “Na wa tatu akamimina bakuli lake ndani ya mito na vibubujiko vya maji. Na hiyo ikawa damu. Na mimi nikasikia malaika aliye na amri juu ya maji akisema: ‘Wewe, Mmoja ambaye yuko na ambaye alikuwako, Mshikamanifu, u mwadilifu, kwa sababu wewe umekata maamuzi haya, kwa sababu wao walimimina damu ya watakatifu na ya manabii, na wewe umewapa damu wanywe. Wao hustahili hiyo.’ Na mimi nikasikia madhabahu ikisema: ‘Ndiyo, Yehova Mungu, Mweza Yote, ya kweli na ya uadilifu ni maamuzi yako ya hukumu.’”—Ufunuo 16:4-7, NW.
7. Ni nini kinachotolewa picha na “mito na vibubujiko vya maji”?
7 Hii “mito na vibubujiko vya maji” ni picha ya yale yaitwayo eti machimbuko ya kisasa hivi ya mwongozo na hekima ambayo hukubaliwa na ulimwengu huu, kama vile falsafa za kisiasa, kiuchumi, kisayansi, kielimu, kijamii, na kidini ambazo huongoza matendo na maamuzi ya binadamu. Badala ya kutegemea Yehova, kwa ajili ya ukweli wenye kutoa uhai, ambaye ndiye Kibubujiko cha uhai, wanadamu ‘wamejichongea wenyewe visima vilivyovunjika’ nao wamekunywa sana “hekima ya ulimwengu huu [ambayo] ni upumbavu kwa Mungu.”—Yeremia 2:13; 1 Wakorintho 1:19; 2:6; 3:19; Zaburi 36:9, NW.
8. Ni katika njia zipi aina ya binadamu imejiletea hatia ya damu?
8 “Maji” kama hayo yaliyochafuliwa yameongoza wanadamu kuwa na hatia ya damu, mathalani, katika kuwatia moyo wamwage damu kwa kadiri kubwa katika vita ambavyo karne iliyopita vilitwaa maisha zaidi ya milioni mia moja. Hususa katika Jumuiya ya Wakristo, ambako vililipuka vita viwili vya ulimwengu, wanadamu wamekuwa “katika uharaka wa kumwaga damu isiyo na hatia,” na hiyo imetia ndani damu ya mashahidi wa Mungu mwenyewe. (Isaya 59:7; Yeremia 2:34, NW) Aina ya binadamu imejiletea pia hatia ya damu kwa kutumia vibaya kiasi kikubwa mno cha damu kwa ajili ya kutia mishipani, katika kukiuka sheria za Yehova za uadilifu. (Mwanzo 9:3-5; Walawi 17:14; Matendo 15:28, 29) Kwa sababu hiyo, kupitia kutiwa damu mishipani, tayari wao wamevuna sikitiko la kuwa na UKIMWI, ugonjwa wa kufura ini, na magonjwa mengine. Lipo kamili kwa ajili ya hatia ya damu litakuja karibuni wakati wakiukaji watakapolipa adhabu iliyo kuu zaidi, wakikanyagwa katika “shinikizo la divai ya kasirani ya Mungu.”—Ufunuo 14:19, 20, NW.
9. Kumiminwa kwa bakuli la tatu kunahusu nini?
9 Katika siku ya Musa, wakati Mto Naili ulipogeuzwa kuwa damu, Wamisri waliweza kuendelea kuwa hai kwa kutafuta machimbuko mengine ya maji. (Kutoka 7:24) Ingawa hivyo, leo, katika pindi ya tauni hii ya kiroho, hakuna mahali katika ulimwengu wa Shetani ambako watu wanaweza kupata maji yenye kutoa uhai. ‘Kumiminwa’ kwa bakuli hili la tatu kunahusu kupiga mbiu kwamba “mito na vibubujiko vya maji” vya ulimwengu viko kama damu, vikileta kifo cha kiroho kwa wote wanaoyanywa. Watu wasipomwendea Yehova, wanavuna hukumu yake mbaya.—Linga Ezekieli 33:11.
10. “Malaika aliye na amri juu ya maji” anajulisha nini, na ni ushahidi gani ambao “madhabahu” inaongezea?
10 “Malaika aliye na amri juu ya maji,” yaani, malaika amiminaye bakuli hili juu ya maji, anatukuza Yehova kuwa ndiye Hakimu wa Ulimwengu Wote Mzima, ambaye maamuzi yake ya uadilifu ni kamili. Kwa hiyo, yeye anasema juu ya hukumu hii: “Wao hustahili hiyo.” Pasipo shaka, huyo malaika alijionea mwenyewe umwagaji-damu mwingi na ukatili uliochochewa na mafundisho bandia na falsafa za ulimwengu huu mbovu kwa muda wa maelfu mengi ya miaka. Kwa sababu hiyo, yeye anajua kwamba uamuzi wa hukumu wa Yehova ni wa haki. Hata “madhabahu” ya Mungu inasema kwa mpaazo. Kwenye Ufunuo 6:9, 10, nafsi za wale ambao waliuawa kiimani husemwa kuwa kwenye msingi wa madhabahu hiyo. Kwa hiyo “madhabahu” inaongeza ushahidi wenye nguvu nyingi kwa habari ya haki na uadilifu wa maamuzi ya Yehova.a Hakika, inawafaa wale ambao wamemwaga na kutumia vibaya damu wenyewe wanyweshwe damu kinguvu, kama ufananisho wa Yehova kuwahukumia kifo.
-
-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 224]
“Ndani ya Mito na Vibubujiko”
Tauni ya tatu imefunua “mito na vibubujiko vya maji” kwa taarifa kama zifuatazo:
“Viongozi wa kidini, wanaodai kuwa walimu wa mafundisho [ya Kristo], wametakasa vita na kuifanya kuwa kitu kitakatifu. Wao wamependezwa kuwa na taswira zao na sanamu-umbo zionyeshwe kando kwa kando na zile za mashujaa wenye kumwaga damu.”—The Watch Tower, Septemba 15, 1924, ukurasa 275.
“Uwasiliano na roho msingi wao ni utokweli mkubwa, uwongo wa kuendelea kuishi baada ya kifo na kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu.”—What Do the Scriptures Say About “Survival After Death?,” 1955, ukurasa 51.
“Falsafa za kibinadamu, wananadharia wa kisiasa, watengenezaji jamii, washauri wa kiuchumi na wateteaji wa mapokeo ya kidini hawakutokeza burudiko lolote halisi lenye kutoa uhai. Maji kama hayo hata yameongoza wanywaji kuhalifu sheria ya Muumba kuhusu utakatifu wa damu na kujitia katika minyanyaso ya kidini.”—Azimio lililokubaliwa kwenye “Habari Njema za Milele” Mkusanyiko wa Kimataifa, 1963.
“Si wokovu wa kisayansi, bali uangamivu wa jamii ya kibinadamu ndilo jambo la kutarajiwa kutoka kwa mwanadamu mwenyewe. . . . Sisi hatuwezi kutegemea wasaikolojia na wasaikayatristi wote wa ulimwengu wabadili njia ya kufikiri ya aina ya binadamu . . . Sisi hatuwezi kutegemea kani ya polisi yoyote ya kimataifa ifanyizwe . . . kufanya dunia hii kuwa mahali salama pa kuishi.”—Saving the Human Race—In the Kingdom Way, 1970, ukurasa 5.
-