-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kuunguza Wanadamu kwa Moto
11. Ni nini iliyo shabaha ya bakuli la nne la kasirani ya Mungu na hutukia nini linapomiminwa?
11 Shabaha ya bakuli la nne la kasirani ya Mungu ni jua. Yohana atuambia sisi: “Na wa nne akamimina bakuli lake juu ya jua; na jua likapewa ruhusa ya kuunguza wanadamu kwa moto. Na wanadamu wakaunguzwa kwa joto kubwa, lakini wao walikufuru jina la Mungu, ambaye ana mamlaka juu ya tauni hizi na wao hawakutubu ili wampe yeye utukufu.”—Ufunuo 16:8, 9, NW.
12. Ni nini lililo “jua” la ulimwengu huu, na jua hili la ufananisho lapewa ruhusa gani?
12 Leo, kwenye huu “umalizio wa mfumo wa mambo,” ndugu za kiroho za Yesu ‘hung’aa kwa uangavu kama jua katika ufalme wa Baba yao.’ (Mathayo 13:40, 43, NW) Yesu mwenyewe ndiye “jua la uadilifu.” (Malaki 4:2, NW) Ingawa hivyo, aina ya binadamu, ina “jua” layo yenyewe, watawala wayo yenyewe ambao hujaribu kung’aa katika kupinga Ufalme wa Mungu. Ule mpigo wa nne wa tarumbeta ulitangaza kwamba ‘jua, mwezi, na nyota’ katika mbingu za Jumuiya ya Wakristo kwa kweli ni machimbuko ya giza, si ya nuru. (Ufunuo 8:12, NW) Bakuli la nne la kasirani ya Mungu huonyesha sasa kwamba “jua” la ulimwengu lingekuwa lenye joto sana isivyovumilika. Wale wanaotegemewa kuwa viongozi kama jua ‘wangeunguza’ aina ya binadamu. Hiyo ruhusa ingepewa kwa jua la ufananisho. Kwa maneno mengine, Yehova angeruhusu hilo kuwa sehemu ya hukumu yake yenye moto juu ya aina ya binadamu. Ni katika njia gani kuunguzwa huku kumetukia?
13. Ni katika njia gani watawala wa ulimwengu huu walio ufananisho wa jua ‘wameunguza’ aina ya binadamu?
13 Baada ya vita ya ulimwengu ya kwanza, watawala wa ulimwengu huu walifanyiza Ushirika wa Mataifa katika jitihada ya kutatua tatizo la ulimwengu la usalama, lakini huu ulishindwa. Kwa hiyo aina nyingine za utawala wa kujaribia zilionjwa, kama vile Ufashisti na Unazi. Ukomunisti uliendelea kupanuka. Badala ya fungu la aina ya binadamu kuwa bora, hao watawala walio kama jua katika mifumo hiyo wakaanza ‘kuunguza aina ya binadamu kwa joto kubwa.’ Vita vya wenyewe kwa wenyewe katika Hispania, Ethiopia, na Manchuria viliongoza kwenye vita ya ulimwengu ya pili. Historia ya ki-siku-hizi hurekodi kwamba Mussolini, Hitla, na Stalini wakiwa madikteta wakawa na daraka la moja kwa moja na lisilo la moja kwa moja la vifo vya makumi ya mamilioni, kutia ndani wengi wa wanataifa wao wenyewe. Hivi majuzi zaidi, mipambano ya kimataifa au ya wenyewe kwa wenyewe ‘imeunguza’ watu wa nchi kama vile Vietnamu, Kampuchea, Irani, Lebanoni, na Ailandi, pamoja na mabara mengine katika Amerika ya Kilatini na Afrika. Ongezea hayo ule mng’ang’ano wenye kuendelea kati ya mataifa yenye nguvu zaidi, ambayo silaha zayo za nyukilia zenye kutia hofu sana zinaweza kuteketeza aina ya binadamu yote. Katika hizi siku za mwisho, hakika binadamu wamewekwa katika hatari ya kuunguzwa na “jua,” watawala wao wasio waadilifu. Kumiminwa kwa bakuli la nne la kasirani ya Mungu kumelenga barabara mambo haya ya hakika ya historia, na watu wa Mungu wameyapigia mbiu kotekote duniani.
14. Mashahidi wa Yehova wamefundisha nini bila ugeugeu kuwa ndio ufumbuzi pekee wa matatizo ya aina ya binadamu, na kwa itikio gani kwa aina ya binadamu kwa ujumla?
14 Mashahidi wa Yehova wamefundisha bila ugeugeu kwamba ufumbuzi pekee wa matatizo magumu ya aina ya binadamu ni Ufalme wa Mungu, ambao kupitia huo Yehova anakusudia kutakasa jina lake. (Zaburi 83:4, 17, 18; Mathayo 6:9, 10) Hata hivyo, aina ya binadamu kwa ujumla imeziba sikio kwa ufumbuzi huu. Wengi ambao wanakataa Ufalme huo, wanakufuru jina la Mungu pia, hata kama vile Farao alivyofanya wakati alipokataa kukiri enzi kuu ya Yehova. (Kutoka 1:8-10; 5:2) Wakiwa hawapendezwi na Ufalme wa Kimesiya, wapinzani hawa wanachagua kutaabika chini ya “jua” kali lao wenyewe la utawala wa kibinadamu wenye uonevu.
-
-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 225]
“Juu ya Jua”
Huku “jua” la utawala wa kibinadamu likiwa ‘limeunguza’ aina ya binadamu wakati wa siku ya Bwana, jamii ya Yohana, imekuwa ikivuta uangalifu kwenye yanayotukia, kwa taarifa kama zifuatazo:
“Leo Hitla na Mussolini, madikteta wenye amri peke yao, wanatisha amani ya ulimwengu kwa ujumla, na wanaungwa mkono kikamili na jamii ya mapadri wa Katoliki ya Roma katika uharibifu wao wa uhuru.”—Fascism or Freedom, 1939, ukurasa 12.
“Muda wote wa historia sera iliyofuatwa na madikteta wa kibinadamu imekuwa, Tawala au angamiza! Lakini kirekebi cha kutumiwa sasa na Mfalme aliyewekwa na Mungu, Yesu Kristo, kwenye dunia yote, ni, Tawalwa au uangamizwe.”—When All Nations Unite Under God’s Kingdom, 1961, ukurasa 23.
“Tangu 1945 zaidi ya watu milioni 25 wameuawa katika vita 150 vilivyopiganwa kuzunguka dunia.”—Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1980, ukurasa 6.
“Mataifa kuuzunguka ulimwengu . . . hayajali sana daraka la kimataifa au amri za mwenendo. Ili kutimiza miradi yao, mataifa mengine yana maoni ya kwamba yana haki kabisa kutumia njia zo zote yanazoziona kuwa lazima—kuchinja watu kwa wingi, kuua, kuteka nyara, kulipua makombora, na kadhalika . . . Ni kwa muda gani mataifa yataendelea kuvumiliana katika mwendo huo wa upumbavu na usiofaa?”—Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1985, ukurasa 4.
-