-
Kukubali Mialiko ya Yehova HuthawabishaMnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 1
-
-
Baada ya kukaa Itu kwa mwaka mmoja hivi, nilipokea mwaliko kupitia telegramu wa kwenda kufanya kazi kwa muda kwenye Betheli, ambayo ni ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Rio de Janeiro. Kazi hiyo ilihusiana na matayarisho ya kusanyiko la kitaifa. Nilikubali mwaliko huo kwa furaha.
Migawo Zaidi na Magumu Mengi Zaidi
Kulikuwa na kazi ya kutosha Betheli, na nilifurahia kusaidia kwa njia yoyote ile. Ilithawabisha kama nini kuhudhuria mazungumzo ya andiko la kila siku na Funzo la Mnara wa Mlinzi kila Jumatatu jioni! Niliguswa moyo sana na sala za kutoka moyoni za Otto Estelmann na washiriki wengine wenye uzoefu wa familia ya Betheli.
Baada ya kusanyiko la kitaifa, nilifunganya virago kurudi Itu, lakini nilishangaa wakati mtumishi wa ofisi ya tawi, Grant Miller, aliponipa barua ya kunialika niwe mshiriki wa kudumu wa familia ya Betheli. Nilikaa chumba kimoja na Dada Hosa Yazedjian, ambaye angali anatumikia katika Betheli ya Brazili. Siku hizo Wanabetheli walikuwa wachache—tulikuwa 28 tu—na sote tulikuwa marafiki sana.
Katika mwaka wa 1964, João Zanardi, mhudumu wa wakati wote aliyekuwa kijana, alikuja Betheli kuzoezwa. Kisha akapewa mgawo wa kuwa mtumishi wa mzunguko au mwangalizi asafiriye katika eneo lililokuwa karibu. Tulikutana mara kwa mara alipokuja Betheli kutoa ripoti zake. Mtumishi wa Betheli alimruhusu João awe anahudhuria funzo la familia ya Betheli Jumatatu jioni, hivyo tuliweza kuwa na wakati mwingi pamoja. Mimi na João tulioana Agosti 1965. Nilifurahi kujiunga na mume wangu katika kazi ya kuzunguka.
-
-
Kukubali Mialiko ya Yehova HuthawabishaMnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 26]
Nikiwa na familia ya Betheli ya Brazili mwaka wa 1963
-