-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Brazili
Dereva wa teksi ya pikipiki ambaye alipokea trakti Habari za Ufalme aliibandika nyuma ya koti lake kwa siku kadhaa na hivyo watu wengi wakaiona. Abiria walilazimika kusoma ukurasa wa kwanza walipokuwa wakisafirishwa.
Dada wawili nchini Brazili walipokaribia nyumba fulani walishtuka kuona kibandiko kilichosema, “Unaweza kuingia, lakini hutatoka ukiwa hai.” Wakiwa na woga waliwauliza ndugu wawili wafanye nini. Ndugu hao waliamua kwenda kwenye nyumba hiyo. Baada ya kusali wapate mwongozo wa Yehova, ndugu hao walipiga makofi ili mwenye nyumba awasikie. Mwenye nyumba, ambaye alikuwa polisi, alikubali trakti Habari za Ufalme. Alieleza kwamba alikuwa akikarabati nyumba yake na alikuwa na vifaa vingi vya ujenzi upande wa nyuma wa nyumba. Kwa hiyo aliweka kibandiko hicho ili kuwaogopesha wezi. Wahubiri hao waliporudi kumtembelea, alikubali kujifunza Biblia.
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 9]
Kweli Ilikuwa Kampeni ya Ulimwenguni Pote
Watu kadhaa katika sehemu mbalimbali walijiuliza ikiwa kweli trakti Habari za Ufalme ilikuwa ikisambazwa ulimwenguni pote. Kwa mfano, mwenye nyumba fulani huko Brazili ambaye alikuwa na shaka alimwambia mhubiri angoje ampigie simu rafiki yake huko Marekani ili ajue ikiwa alikuwa ameipata. Rafiki yake akamjibu, “Ndiyo, nimepata nakala moja dakika kumi zilizopita.” Akiwa ameshangaa, mwenye nyumba huyo alikubali trakti Habari za Ufalme na akaahidi kuisoma kwa makini.
-