Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini Zote
    Huduma ya Ufalme—1998 | Februari
    • 17 Kuwatolea Wabuddha Ushahidi: (Ona sura ya 6 katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.) Itikadi za Kibuddha za mwamini mmoja zatofautiana sana na zile za mwamini mwingine. Badala ya kutetea kuwapo kwa Muumba mwenye utu, Ubuddha humwona mwanamume Mhindi Buddha Gautama, wa karne ya sita K.W.K., kuwa mfano bora wa kidini. Mara ya kwanza Gautama alipoona mwanamume mgonjwa, mwanamume mzee, na mwanamume aliyekufa, alipatwa na maumivu makali kuhusu maana ya uhai. ‘Je, wanadamu walizaliwa wateseke, wazeeke, na kufa tu?’ alijiuliza. Bila shaka, twaweza kujibu maswali hayo kwa ajili ya Wabuddha wenye moyo mweupe ambao wanataka kujua majibu.

      18 Unaposema na Wabuddha, tumia tu ujumbe ulio chanya na kweli zilizo wazi zipatikanazo katika kitabu kitakatifu kilicho kikubwa zaidi ya vyote, Biblia. Kama vile watu wengine walio wengi, Wabuddha wanapendezwa sana na amani, adili, na maisha ya familia, na mara nyingi wao hukaribisha mazungumzo juu ya mambo hayo. Hilo laweza kuongoza katika kukazia kwako Ufalme kuwa utatuzi halisi wa matatizo ya wanadamu.

      19 Katika sehemu fulani za mji mkuu za Afrika Mashariki, kumekuwa na Wachina kadhaa ambao huamini Ubuddha na falsafa nyinginezo za Kimashariki. Wengi wanafanya kazi katika miradi tofauti-tofauti. Kwa mfano, dada mmoja katika Montana, Marekani, alipomwona mwanamume Mchina katika duka la kuuzia mboga, alimpa trakti katika lugha yake na kumtolea funzo la Biblia. Yeye alisema: “Wamaanisha Biblia Takatifu? Nimekuwa nikiitafuta maishani mwangu mwote!” Alianza kujifunza juma hilo na kuanza kuhudhuria mikutano yote. Vivyo hivyo, wahubiri fulani katika eneo letu wameweza kuanzisha mafunzo ya Biblia na Wachina fulani.

      20 Kwa muda wa zaidi ya mwongo moja, dada painia katika Nevada amekuwa akifundisha wanafunzi Wachina kweli. Alipokuwa akihubiri jengo moja lililokuwa na vyumba vinane vilivyokaliwa na wanafunzi hawa, alisali kwa Yehova amsaidie kuanzisha funzo katika kila chumba. Katika majuma mawili alikuwa akijifunza na angalau mwanafunzi mmoja katika kila chumba. Mfikio ufanyao kazi vizuri kwake ni kusema kwamba amepata miongoni mwa wanafunzi hao hangaiko moja linalofanana—wote wanataka amani na furaha. Kisha yeye huuliza kama hilo ni hangaiko lao pia. Sikuzote wao hukubali. Yeye huelekeza uangalifu wao kwenye broshua Lasting Peace and Happiness—How to Find Them, ambayo imekusudiwa Wachina. Baada ya kujifunza masomo matano tu, mwanafunzi mmoja alimwambia amekuwa akitafuta kweli kwa muda mrefu na sasa ameipata.

  • Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini Zote
    Huduma ya Ufalme—1998 | Februari
    • Wabuddha

      “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” (Broshua)

      In Search of a Father (Kijitabu)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki