-
Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya WakristoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na wa kwanza akapuliza tarumbeta yake. Na kukatukia mvua-mawe na moto uliotangamana na damu, nayo ikavurumishwa kwenye dunia; na theluthi moja ya dunia ikateketezwa, na theluthi moja ya miti ikateketezwa, na mimea yote ya chanikiwiti ikateketezwa.” (Ufunuo 8:7, NW)
-
-
Tauni za Yehova juu ya Jumuiya ya WakristoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
18. Ujumbe wa hukumu ya Yehova ulipigiwaje mbiu kwenye mkusanyiko wa 1922 katika Sida Pointi, Ohaiyo?
18 Ujumbe huu wa hukumu unapelekwaje? Kwa kawaida, si kupitia vyombo vya habari, ambavyo ni sehemu ya ulimwengu na mara nyingi husuta “mtumwa” wa Mungu. (Mathayo 24:45) Ulipelekwa kwa njia yenye kujulikana kwenye mkutano wa pili wenye kufanyiza historia wa watu wa Mungu katika Sida Pointi, Ohaiyo, Septemba 10, 1922. Kwa umoja na kwa idili hawa walikubali azimio lililokuwa na kichwa “Sai kwa Waongoza Ulimwengu.” Katika semi zilizo wazi, lilijulisha “dunia” ya ufananisho ya ki-siku-hizi, kama ifuatavyo: “Kwa hiyo sisi tunayaomba mataifa ya dunia, watawala na viongozi wayo, na viongozi wa kidini wote wa migawanyiko yote ya makanisa ya dunia, wafuasi wayo na wafungamani, biashara kubwa-kubwa na wanasiasa wakubwa-wakubwa, watokeze ushahidi katika kuthibitisha msimamo waliouchukua kwamba wao wanaweza kusimamisha amani na ufanisi duniani na kuleta furaha kwa watu; na wakishindwa katika hili, sisi tunawaomba wategee sikio ushahidi ambao sisi tunatoa tukiwa mashahidi kwa ajili ya Bwana, na kisha acheni wao waseme kama ushahidi wetu ni wa kweli au sivyo.”
19. Ni ushahidi gani ambao watu wa Mungu walipelekea Jumuiya ya Wakristo kuhusu Ufalme wa Mungu?
19 Mashahidi hawa walitoa ushahidi gani? Huu: “Sisi tunashikilia na twajulisha kwamba ufalme wa Mesiya ndio ponyo kamili kwa taabu zote za aina ya binadamu nao utaleta amani duniani na nia njema kwa watu, ile tamaa ya mataifa yote; kwamba wale wanaojitoa kwa moyo wa kupenda kwa utawala wake wa uadilifu [ambao] sasa umeanza watabarikiwa kwa amani ya kudumu, uhai, uhuru na furaha isiyokwisha.” Katika nyakati hizi zenye ufisadi, wakati serikali zilizofanywa na binadamu, hasa katika Jumuiya ya Wakristo, zinashindwa kabisa kutatua magumu ya siku hizi, dai hilo la ithibati lenye kupigiwa tarumbeta lina mlio ulio na kani kubwa hata zaidi ya ulivyokuwa katika 1922. Jinsi ilivyo kweli kwamba Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa Kristo wake mwenye kushinda ndio tumaini moja tu na la pekee la aina ya binadamu!
-