Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 2: Maisha ya Kikristo
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 32. Wakristo wanatazamia kupatwa na hali zipi ngumu?

      • “Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao. Wenye furaha ni ninyi, watu wanapowashutumu na kuwatesa na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa sababu yangu. Furahini na kushangilia sana, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwapo kabla yenu.”—Mt. 5:10-12.

      33. Kwa nini ni pendeleo la pekee kubatizwa ili kuwa Shahidi wa Yehova?

      • “Neno lako likawa furaha na shangwe ya moyo wangu, kwa maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Yehova Mungu.”—Yer. 15:16.

  • Mazungumzo ya Kumalizia Pamoja na Wale Wanaotaka Kubatizwa
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • MASWALI KWA AJILI YA WALE WANAOTAKA KUBATIZWA

      Mazungumzo ya Kumalizia Pamoja na Wale Wanaotaka Kubatizwa

      Kwa kawaida, ubatizo hufanywa kwenye makusanyiko ya Mashahidi wa Yehova. Mwishoni mwa hotuba ya ubatizo, msemaji atawaomba wale wanaotaka kubatizwa wasimame na kujibu maswali mawili yafuatayo kwa sauti inayosikika waziwazi:

      1. Je, umetubu dhambi zako, ukajiweka wakfu kwa Yehova, na kukubali njia yake ya wokovu kupitia Yesu Kristo?

      2. Je, unaelewa kwamba ubatizo wako unakutambulisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova anayeshirikiana na tengenezo la Yehova?

      Kujibu maswali hayo ni “tangazo la hadharani” la kwamba wale wanaotaka kubatizwa wana imani katika fidia na kwamba wamejiweka wakfu kwa Yehova kwa moyo wote. (Rom. 10:9, 10) Wale wanaotaka kubatizwa wanapaswa kusali na kufikiria kwa uzito maswali hayo mapema ili waweze kujibu kupatana na usadikisho wao.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki