Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Okoa Maisha ya Mtoto Wako!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Julai 15
    • MICHAEL na Alphina huishi katika bonde la mashambani katikati ya vilima vya kijani kibichi vya KwaZulu-Natal, Afrika Kusini. Walikabili magumu mengi katika kuwalea watoto saba. Kwa utegemezo kamili wa mkewe, Michael alifanya yote aliyoweza katika kutii hii amri ya Biblia kwa akina baba: “Endeleeni kuwalea [watoto wenu] katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.” (Waefeso 6:4) Lakini nyakati nyingine matatizo hutokea.

      Kwa kielelezo, ni jambo la kawaida kwa wachungaji wavulana Waafrika kuchanganya makundi ya ng’ombe za familia zao na zile za familia nyingine ili wawe na wakati wa kucheza pamoja. Nyakati nyingine wao hufanya utundu na huzungumza juu ya mambo ambayo hawapaswi kuyazungumza. Wana wa Michael walipotoka kwenda kuchunga ng’ombe za familia, aliwatolea maagizo makali wasishirikiane na watoto fulani. (Yakobo 4:4) Hata hivyo, aliporudi nyumbani kutoka kazini, nyakati nyingine aliwapata wakifanya hivyo. Tokeo ni kwamba, alilazimika kuwatia nidhamu.—Mithali 23:13, 14.

      Je, wafikiri kwamba Michael alikuwa mkali mno kwa watoto wake? Huenda wengine wakahisi hivyo, lakini Yesu Kristo alisema kwamba “hekima huthibitishwa kuwa yenye uadilifu kwa kazi zayo.” (Mathayo 11:19) Michael na Alphina walitokeza hali yenye upendo nyumbani mwao, wakitumia wakati pamoja na watoto wao na kuwafundisha masimulizi na kweli za Biblia.

      Michael na Alphina wana binti wanne—Thembekile, Siphiwe, Tholakele, na Thembekani. Wote ni wahubiri wa wakati wote wa habari njema ya Ufalme wa Mungu. Wawili wa wanao hutumikia wakiwa waangalizi-wasimamizi katika makutaniko ya Mashahidi wa Yehova. Mwana wao wa tatu, ambaye mkewe pia ni mweneza-evanjeli wa wakati wote, hutumikia akiwa mtumishi wa huduma.

  • Okoa Maisha ya Mtoto Wako!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Julai 15
    • Mama mmoja kutoka Afrika ya Kusini aeleza hivi: “Tangu ile siku ya kwanza binti yetu alienda shuleni, tulimtia moyo asimulie yaliyotukia katika hiyo siku. Kwa kielelezo, ningemwuliza hivi: ‘Ulitumia mapumziko ya chakula cha mchana ukiwa na nani? Niambie juu ya mwalimu wako mpya. Anaonekanaje? Ni utendaji gani ambao umepangwa kwa ajili ya hili juma?’ Siku moja, binti yetu alikuja nyumbani na kusema kwamba mwalimu wa Kiingereza alikuwa akipanga kupeleka darasa kuona sinema ambayo baadaye wangeandika pitio juu yake. Kichwa cha hiyo sinema kilikuwa chenye kutilika shaka. Tulipofanya uchunguzi, tuligundua kwamba haingefaa kwa Mkristo. Tulizungumza juu yake tukiwa familia. Siku iliyofuata binti yetu alimfikia huyo mwalimu, akimweleza kwamba hakutaka kuiona hiyo sinema, kwa kuwa maadili iliyoyaonyesha hayangepatana na itikadi zake za Kikristo. Huyo mwalimu alilifikiria jambo hilo tena na baadaye akamshukuru binti yetu, akisema kwamba hakutaka kuipeleka hilo darasa kuona kitu ambacho angejutia.” Upendezi ambao hawa wazazi walionyesha bila ugeugeu katika wokovu wa binti yao ulizaa matunda mazuri. Yeye ana asili chanya, yenye furaha na sasa anatumikia akiwa mjitoleaji kwenye ofisi ya tawi ya Afrika Kusini ya Watch Tower Bible and Tract Society.

  • Okoa Maisha ya Mtoto Wako!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Julai 15
    • Mwanamume kijana anayetumikia kwenye ofisi ya tawi ya Afrika Kusini ya Watch Tower Bible and Tract Society aeleza hivi: “Nilipokuwa mvulana, nilikuwa nikimsaidia baba yangu kazi za nyumbani. Nilifurahia kumsaidia, kwa sababu tu baba alithamini kikweli yale machache niliyofanya. Alikuwa akitumia huo wakati kuniambia mambo mengi juu ya Yehova. Kwa kielelezo, ninakumbuka Jumamosi moja tulipokuwa tukijitahidi kufyeka nyasi bustanini. Kulikuwa na joto sana. Baba alikuwa akitoa jasho, hivyo nilikimbia na kuleta gilasi mbili za maji na kuyatia barafu. Baba alisema hivi: ‘Mtoto, je, unaona jinsi Yehova alivyo mwenye hekima? Barafu huelea juu ya maji. Ikiwa ingezama, uhai wote ulio chini ya maziwa na vidimbwi ungekufa. Badala ya hivyo, barafu hutumika kama blanketi ya kufunikia! Je, hilo halitusaidii kumjua Yehova vizuri zaidi?’a Baadaye, nilipofungwa kwa ajili ya kudumisha kutokuwamo, nilikuwa na wakati wa kufikiri. Usiku mmoja nikiwa nimeshuka moyo katika seli yangu gerezani, nilikumbuka maneno hayo ya baba. Yalikuwa na maana ilioje! Ningemwabudu Yehova milele ikiwa ningeweza.”

  • Okoa Maisha ya Mtoto Wako!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Julai 15
    • Baba mmoja kutoka Afrika ya Kusini aliye baba wa binti wawili na mwana mmoja aeleza hivi: “Katika pindi nyingi, nilikuwa na fursa za kuzungumza juu ya mambo nyetivu ya kingono hata pamoja na wasichana. Ingawa hivyo, mke wangu alisikiliza kwa uangalifu sana, akitumia kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako. [Ona ukurasa wa 26-31.] Mwanangu alipokuwa na umri wa miaka 12, niliamua kumchukua kwa ajili ya matembezi marefu milimani. Katika pindi hiyo, tulizungumza kinaganaga na kwa urefu juu ya ukuzi wa mwili wa mvulana na kusudi la pekee huo ungetimiza katika ndoa. Nilizungumza naye pia juu ya uhitaji wa kuepuka zoea lenye kushusha la kupiga punyeto na kuwaona wasichana kwa njia yenye heshima na staha—kama awaonavyo mama na dada zake.”

      Thawabu Zenye Shangwe

      Baba na mama ambao wametoka tu kutajwa walifanya kazi kwa bidii na ni wenye furaha kwamba walikuwa na matokeo mazuri katika kulea watoto wao watatu. Wote wakiwa watatu sasa ni watu wazima, ambao wameolewa na Wakristo waaminifu. Mwana wao na wakwe zao wote hutumikia wakiwa wazee katika kutaniko la Kikristo, na wanne katika hao mume na mke wamekuwa waeneza-evanjeli wa wakati wote kwa miaka mingi.

      Ndiyo, wazazi ambao hujitahidi kwa ajili ya wokovu wa watu wa nyumbani mwao waweza kutarajia thawabu yenye shangwe kutokana na watoto ambao huchagua kuitikia mafundisho hayo ya Biblia, kwa maana kitabu cha Mithali 23:24, 25 husema hivi: “Amzaaye mtoto mwenye hekima atamfurahia. Na wafurahi baba yako na mama yako.” Fikiria kwa uangalifu familia kubwa iliyotajwa mwanzoni mwa makala hii. “Nifikiriapo maendeleo ya kiroho ambayo watoto wangu wamefanya,” asema Alphina, “moyo wangu hububujika kwa shangwe.” Wazazi wote Wakristo na wafanye kazi kufikia thawabu hiyo yenye furaha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki