-
Kusitawisha Upendo wa Yehova Katika Mioyo ya Watoto WetuMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
Daraka Letu Mbele ya Yehova
Kufundisha watoto wampende Mungu kwahusisha kusoma na kujifunza Neno lake kwa ukawaida. Kwa kuzingatia jambo hilo, tulifanya funzo la familia kila juma, hasa Jumatatu jioni. Kwa kuwa mtoto wa kwanza na wa mwisho waliachana kwa miaka tisa, mahitaji ya watoto yalitofautiana sana, kwa hiyo hatungeweza kuchunguza habari ileile na wote.
Kwa mfano, tulirahisisha sana mafundisho kwa ajili ya watoto ambao hawakuwa wameanza kwenda shuleni. Karla alizungumza nao andiko moja tu la Biblia, au alitumia picha za vichapo vinavyozungumzia habari ya Biblia. Ningali nakumbuka jinsi nilivyokuwa nikiamshwa asubuhi na watoto wachanga wakipanda juu ya kitanda chetu kutuonyesha picha walizopenda zaidi katika kitabu The New World.a
Karla alisitawisha ustadi wa kufundisha watoto kwa saburi waelewe sababu nyingi zinazofanya tumpende Yehova. Huenda kazi hiyo ikasikika kuwa rahisi, lakini kwa kweli, ilikuwa kazi yenye kuchosha kimwili na kihisia-moyo na ilichukua muda wetu mwingi. Hata hivyo, hatukukata tamaa. Tulitaka kusitawisha upendo huo katika mioyo yao michanga kabla hawajaathiriwa na watu wengine wasiomjua Yehova. Kwa hiyo, tulisisitiza kwamba watoto wetu wahudhurie funzo la familia mara tu walipoanza kuketi.
-
-
Kusitawisha Upendo wa Yehova Katika Mioyo ya Watoto WetuMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
Kuwapa Watoto Uangalifu Waliohitaji
Bila shaka, mambo hayakuwa shwari wakati wote. Kadiri watoto walivyokua, tulitambua kwamba ili kuwasaidia wasitawishe upendo mioyoni mwao tulihitaji kujua ni nini kilicho mioyoni mwao. Hiyo ilimaanisha kuwasikiliza. Nyakati nyingine watoto wetu walitulalamikia, kwa hiyo mimi na Karla, tuliketi chini na kuzungumza pamoja nao. Tulitenga wakati hususa wa nusu saa baada ya funzo la familia. Kila mtu alipewa ruhusa ya kutoa maoni yake waziwazi.
Kwa mfano, Thomas na Gabriele, watoto wetu wachanga zaidi, walihisi kwamba tulikuwa tukimpendelea ndugu yao mkubwa. Wakati mmoja walitueleza maoni yao waziwazi kwa kusema: “Baba, twaona kwamba wewe na Mama sikuzote humruhusu Hans Werner afanye apendavyo.” Mwanzoni, nilishangaa. Hata hivyo, baada ya kufikiria jambo hilo pasipo kupendelea upande wowote, mimi na Karla tulikiri kwamba watoto wetu walikuwa wamesema kweli. Kwa hiyo tukajitahidi kuwatendea sawa watoto wote.
-