Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nilifundishwa Kumpenda Mungu Tangu Utotoni
    Amkeni!—2004 | Oktoba 22
    • Kulea Watoto na Kuwatumikia Wengine

      Binti yetu wa pili, Lilya, alizaliwa mwaka wa 1966. Mwaka mmoja baadaye tulihamia mji wa Belyye Vody, kusini mwa Kazakhstan karibu na mpaka wa Uzbekistan, ambapo kulikuwa na kikundi kidogo cha Mashahidi. Punde si punde, kutaniko likaanzishwa na nikawekwa kutumikia nikiwa mwangalizi-msimamizi. Mnamo 1969, tulipata mwana anayeitwa Oleg, na miaka miwili baadaye, Natasha, ambaye ndiye kitinda mimba. Mimi na Lidiya hatukusahau kamwe kwamba watoto ni urithi kutoka kwa Yehova. (Zaburi 127:3) Tulijadiliana kuhusu jinsi ya kuwalea ili wampende Yehova.

      Hata katika miaka ya 1970, ndugu wengi walikuwa bado katika kambi za kazi ngumu. Makutaniko mengi yalihitaji Wakristo wakomavu ili wasimamie mambo na kutoa mwongozo. Hivyo, Lidiya alitimiza mengi katika kuwalea watoto wetu, nyakati nyingine akitimiza wajibu wake na wangu, huku nikitumikia nikiwa mwangalizi anayesafiri. Nilitembelea makutaniko huko Kazakhstan, na pia katika jamhuri za Sovieti za Turkmenistan, Tajikistan, na Uzbekistan. Wakati huohuo, nilifanya kazi ili kuruzuku familia, na Lidiya na watoto waliniunga mkono.

      Ingawa mara nyingine sikurudi nyumbani kwa majuma kadhaa, nilijitahidi kuwapenda watoto wangu na kuwasaidia kukua kiroho. Mimi na Lidiya tulimwomba Yehova kwa bidii awasaidie watoto wetu, nasi tukazungumza nao kuhusu kushinda tatizo la kuwaogopa wanadamu na kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Mungu. Kama mke wangu hangenisaidia, singeweza kutimiza mgawo wangu nikiwa mwangalizi anayesafiri. Lidiya na dada wengine hawakuwa “kikundi dhaifu” kama vile yule ofisa wa jeshi alivyokuwa amedai. Walikuwa wenye nguvu sana kiroho!—Wafilipi 4:13.

  • Nilifundishwa Kumpenda Mungu Tangu Utotoni
    Amkeni!—2004 | Oktoba 22
    • Familia Yetu Leo

      Tunamshukuru Mungu sana kwa kutusaidia kuwafundisha watoto wetu kweli za Biblia! Binti yetu mkubwa Valentina aliolewa, naye na mume wake wakahamia Ingelheim, Ujerumani, mwaka wa 1993. Wana watoto watatu ambao ni Mashahidi wa Yehova waliobatizwa.

      Binti yetu wa pili, Lilya, ana familia pia. Yeye pamoja na mume wake ambaye ni mzee wa kutaniko la Belyye Vody, wanawasaidia watoto wao wawili kumpenda Mungu. Oleg alimwoa Natasha, dada kutoka Moscow, nao wanatumikia katika ofisi ya tawi iliyo karibu na St. Petersburg, nchini Urusi. Katika mwaka wa 1995, binti yetu mdogo Natasha aliolewa, naye pamoja na mume wake wanatumikia kutaniko la Kirusi, nchini Ujerumani.

      Mara kwa mara familia yetu hupanga kuwa pamoja. Watoto wetu huwaeleza watoto wao jinsi “Mama” na “Baba” walivyomtii Yehova na kuwasaidia watoto wao kumpenda na kumtumikia Mungu wa kweli, Yehova. Mazungumzo hayo huwasaidia wajukuu wetu kukua kiroho. Mjukuu wetu mdogo, anafanana sana na mimi nilipokuwa na umri kama wake. Nyakati nyingine yeye huketi pajani pangu na kuniomba nimsimulie hadithi ya Biblia. Mimi hutokwa na machozi ninapokumbuka jinsi nilivyoketi pajani pa Babu na jinsi alivyonisaidia kumpenda na kumtumikia Muumba wetu Mtukufu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki